• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mpwapwa District Council
Mpwapwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
        • Fedha
        • Biashara
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Mali asili
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Usafi na Mazingira
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Habari Mawasiliano na Tehama
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Nyuki
    • Mamlaka
      • Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mpwapwa
      • Mamlaka ya Maji Mpwapwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashuri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa mbali mbali
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo mbali mbali
    • Simulizi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video mbali mbali
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Wamiliki wa Nyumba za Kulala Wageni Waonywa

Posted on: May 25th, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Jabir Shekimweri amelazimika kuitisha kikao cha dharura na wamiliki wa nyumba za kulala wageni (guest, lodge and hotel) baada ya kutoridhishwa na mwenendo wa utoaji huduma wa nyumba hizo za wageni wilayani Mpwapwa. Kikao hicho kimewahusisha, wamiliki wa nyumba za kulala  wageni, maafisa mazingira, afisa biashara, maafisa tarafa na baadhi ya watendaji wa kata. Vilevile makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Mpwapwa Mhe. George Fuime na Kaimu Mkurugenzi wa Wilaya ya Mpwapwa wamehudhuria katika kikao hicho.

Wajumbe wa kikao cha wamiliki wa nyumba za kulala wakifuatilia maagizo na maelekezo ya mkuu wa wilaya ya Mpwapwa (Picha na: Shaibu J. Masasi, Afisa TEHAMA - Mpwapwa)

Mhe. Shekimweri katika hotuma yake ya ufunguzi wa kikao hicho amesema kuwa kwa taarifa alizonazo kuna baadhi ya wamiliki wa nyumba za kulala wageni wanaendeleza kujenga guest zingine kiholela bila kufuata taratibu, wengine wanahifadhi machangudoa, kukaribisha watoto chini ya umri wa miaka 18 kama wateja wao, kutoa huduma ya chapu chapu (short time) na kuruhusu vibaka kuwaibia wateja. Aidha ameongeza kuwa baadhi ya nyumba za kulala wageni hazi zingatii kanunu za usafi wa mazingira hasa usafi wa choo, chumba, mashuka na mazingira ya nje. Pia ameonya hatasita kumchukulia hatua mmilikia atakaebainika anaenda kinyume na kanunu za umiliki wa nyumba hizo. 

Mmoja wa wamiliki wa nyumba za kulala wageni akidai kuwa wahudumu wao ndio wanaowahujumu hivyo kuanzia leo watawasimamia wahudumu na hakutakuwa tena na huduma za chapuchapu na mambo mengine yasiofaa. (Picha na: Shaibu J. Masasi, Afisa TEHAMA - Mpwapwa)

Akitolea mfano Mhe. Shekimweri kuwa nyumba za kulala wageni za Zanzibar hawaruhusu wateja kulala katika chumba kimoja kama jinsia zao ni sawa, pia kama mwanamke na mwanaume wasio na vyeti vya ndoa na watoto wadogo waliochini ya umri wa miaka 18 bila mzazi wa jinsia sawa na ya mtoto huyo. Hii imepunguza sana hali ya vitendo vialifu na unyanyasaji wa kingono kwa watoto. Hivyo ametoa wito kwa wanamiliki wa nyumba za kulala wageni wilayani Mpwapwa waige mbinu hizo.

Vilevile Mkuu wa Wilaya huyo amewataka wamiliki hao kutokutumia vitabu viwili mpaka vitatu kwa lengo la kutoa takwimu za uongo kwa maafisa mapato na kupoteza mapato, ikibainika hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhini yao.

Mwisho, sambamba na maagizo hayo Mkuu wa Wilaya amewakumbusha wamiliki hao wa nymba za kulala wageni kuwa kuna ujio wa reli ya treni ya mwendo kasi (Standard Gauge) yenye fursa kemkem itakuwa na kituo wilayani Mpwapwa kata ya Gulwe, hivyo wawekeza sana katika nyumba bora, nzuri na za kisasa za kulala wageni, vyakula na biashara mbalimbali kwa kuwa tunatarajia kuwa na wageni wengi sana kutoka nje na ndani ya nchi ya Tanzania kufika Mpwapwa.

Mmoja wa wamiliki wa nyumba za kulala wageni akidai kuwa hakuwa anajua kuwa reli ya mwendokasi itakuwa na kituo mpwapwa na hivyo amemshukuru Mkuu wa Wilaya Mhe. Jabir Shekimweri kwa kuwafafanulia fursa zitakazopatikana baada ya reli kukamilika. (Picha na: Shaibu J. Masasi, Afisa TEHAMA - Mpwapwa)

Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye usahili MpwapwaDC June 27, 2022
  • Tangazo la nafasi za kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa. 2022 April 20, 2022
  • Tangazo la Nafasi za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa May 2022 May 31, 2022
  • Tangazo la kuahirishwa kwa Usahili Halmashauri ya Mpwapwa June 22, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • NORISH NA WAKULIMA WILAYA YA MPWAPWA

    May 06, 2025
  • VIONGOZI KUTOKA OFISI YA MAKAMU WA RAIS ZANZIBAR WATEMBELEA MIRADI YA MFUKO WA JIMBO MPWAPWA

    May 09, 2025
  • FUM YAFANYA ZIARA MIRADI YA KIMAENDELEO

    April 29, 2025
  • MAADHIMISHO YA MEI MOSI YAFANYIKA SINGIDA

    May 01, 2025
  • Tazama zote

Video

Video ya Mpango wa Uuzaji wa Viwanja Eneo la Mazae Block "E" katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa -2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa
  • Muundo wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani
  • Ratiba ya Vikao vya Madiwani

Viunganishi Linganishi

  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Wizara ya Fedha na Mipango
  • Utumishi portal
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu Teknolojia na Sayansi
  • Sekretarieti ya Ajira

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mpwapwa - Dodoma, Tanzania

    Anwani: S.L.P 12

    Simu: 255 26 2320122/2320

    Simu ya Kiganjani: 0684705551

    Barua pepe: info@mpwapwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovutii

Copyright © 2021 Mpwapwa District Council . All rights reserved.