• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mpwapwa District Council
Mpwapwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
        • Fedha
        • Biashara
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Mali asili
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Usafi na Mazingira
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Habari Mawasiliano na Tehama
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Nyuki
    • Mamlaka
      • Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mpwapwa
      • Mamlaka ya Maji Mpwapwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashuri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa mbali mbali
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo mbali mbali
    • Simulizi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video mbali mbali
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Health

SEKTA YA AFYA

Huduma za Afya

Wilaya ina Hospitali moja (1), Vituo vya Afya vinne (4), zahanati 52 kati ya hizo za Serikali ni 48, mashirika 3 na binafsi moja (1). Vijiji 46 kati ya vijiji 113 vilivyopo Wilayani vina vituo vya huduma ya afya sawa na asilimia 40.7 ya mahitaji yote.

Jedwali Na.1;  Idadi ya vituo vya kutolea huduma

Na
Aina
Mahitaji
Zilizopo
Pungufu
% ya upungufu
1
Hospital
1
1
0
0
2
Vituo vya Afya
33
4
29
87.9
3
Zahanati
113
52
61
53.9


Halmashauri ya wilaya ya Mpwapwa ina jumla ya vijiji 113 na ili kuhakikisha kila kijiji kinakuwa na Zahanati na kila kata inakuwa na kituo cha afya, Halmashauri ya wilaya ya Mpwapwa inaendelea kutenga fedha katika bajeti yake kila mwaka pia kushirikisha nguvu za wananchi kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya, majengo ya Zahanati pamoja na nyumba za watumishi katika maeneo mbalimbali. Kwasasa tunaendelea na ujenzi wa Zahanati tisa (9) , Majengo ya kutolea huduma (OPD) vituo vya afya vine (4) na Nyumba za watumishi mbili (2).

Magonjwa ya Mlipuko 

Idara ya afya kupitia timu ya  wataalamu wake kuanzia tarehe 16 Februari 2016,  walienda kufuatilia taarifa za wagonjwa wa kuharisha na kutapika katika wilaya, sambamba na ugawaji wa dawa na vifaa tiba vya kupambana na kuzuia kuharisha na kutapika katika zahanati za kutolea huduma. Hata hivyo wagonjwa watatu waliripotiwa kufariki hadi tarehe 16 Machi 2016

Chanjo

Katika kukabiliana na tatizo la vifo vya akina mama wajawazito pamoja na watoto wachanga na walio chini ya miaka mitano, mkakati uliopo ni kuhakikisha kwamba akina mama wote wenye uwezo wa kuzaa pamoja na watoto chini ya miaka mitano wanapata chanjo ili kujikinga na magonjwa yanayozuilika. Hali ya uchanjaji inaridhisha kwa kuwa kwa watoto chini ya miaka mitano uchanjaji ni zaidi ya asilimia 80 na kwa akinamama wajawazito ni zaidi ya asilimia 90

Jitihada zilizopo katika kukabiliana na vifo vya akina mama na watoto

Kuendelea kuelimisha Jamii juu ya afya ya uzazi na uzazi salama kwa kushirikisha wanaume

Kuendelea kuelimisha wakunga wa jadi kuwasindikiza wajawazito katika vituo vya kutolea huduma na kuendelea kutoa motisha wa fedha kwa wakunga wa jadi kwa kutumia fomu maalum  inayotumika kumpa rufaa mjamazito kutoka kwa mkunga wa jadi ili kwenda kwenye vituo vya afya.

Kuendelea kuhamasisha mama wajawazito wenye vidokezo vya hatari kwenda kwenye nyumba ya kusubiria kujifungua yaani Chigonela.

Programu za afya - Mfuko wa Afya ya Jamii

Jumla ya kaya 15,984 kati ya 66,316 tayari zimejiunga na mfuko. Mapato yanayotokana na Mfuko huu yametumika kuboresha huduma zitolewazo katika vituo vya huduma kama vile ununuzi wa vitendea kazi, madawa, ukarabati na ujenzi wa miundombinu ya vituo husika.

Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa

Wanachama wameendelea kuongezeka kadri watumishi wapya wanavyoajiriwa na vilevile huduma zimekuwa zikitolewa na kuboreshwa hata pale Hospitali au vituo vya afya vinapokuwa havina dawa wanachama wanapewa fomu maalumu kwenda kupata dawa au vifaa tiba katika maduka ya dawa muhimu ya watu binafsi.

Programu za UKIMWI

Utekelezaji wake ni wa kuridhisha japo kumekumbwa na tatizo la vitendea kazi. Aidha kumekuwa na changamoto ya kutokuwepo kwa wakati kwa dawa za kupunguza makali ya UKIMWI (ARV).  Huduma hii inatolewa katika vituo 5.

Katika kuendeleza vita dhidi ya UKIMWI, elimu na semina zinatolewa kwa vijana, wazee na makundi maalum.  Serikali ya Marekani kupitia Shirika lisilo la kiserikali la TUNAJALI imejenga majengo ya Kliniki za matibabu na uangalizi wa wagonjwa wa UKIMWI katika vituo vya kutolea huduma za afya.

Programu za Kifua Kikuu

Matibabu na upimaji wa wagonjwa unaendelea pamoja na ushirikishwaji wa mradi wa UKIMWI kwa wagonjwa wenye magonjwa yote mawili. Huduma inatolewa katika vituo 5.

Vifaa vya kuhudumia wagonjwa

Serikali imekuwa ikitoa vifaa kwa ajili kutolea huduma mbalimbali katika vituo vya huduma kulingana na aina na ngazi ya kituo. Hivi sasa hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ina CD4 machine 1, X-ray machine 1, Ultra-sound machine 1, Biochemical machine 1, Kiti maalumu kwa ajili ya kutolea matibabu ya meno pamoja na vifaa vinginevyo vya tiba na uchunguzi,hata hifyo bado mahitaji ya vifaa ni makubwa

Upatikanaji wa madawa

Serikali kupitia Mpango wake wa ILS (Intergrated Logistic System) imekuwa ikitoa madawa pamoja na vifaa tiba katika vituo vyote vya kutolea huduma vya Serikali kulingana na mahitaji ya kituo husika na hivyo kuvifanya vituo vya huduma kuwa na dawa pamoja na vifaa vya kutosha.  

Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye usahili MpwapwaDC June 27, 2022
  • Tangazo la nafasi za kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa. 2022 April 20, 2022
  • Tangazo la Nafasi za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa May 2022 May 31, 2022
  • Tangazo la kuahirishwa kwa Usahili Halmashauri ya Mpwapwa June 22, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • NENDENI MKAITANGAZE SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    May 24, 2025
  • KIKAO KAZI CHA MAAFISA HABARI WA MIKOA, HALMASHAURI NA TAASISI ZA OFISI YA RAIS TAMISEMI CHAFANYIKA DODOMA

    May 23, 2025
  • AWAMU YA PILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA LAWADIA RASMI MPWAPWA

    May 14, 2025
  • NHIF WATOA MAFUNZO KWA MADIWANI

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

Video ya Mpango wa Uuzaji wa Viwanja Eneo la Mazae Block "E" katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa -2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa
  • Muundo wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani
  • Ratiba ya Vikao vya Madiwani

Viunganishi Linganishi

  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Wizara ya Fedha na Mipango
  • Utumishi portal
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu Teknolojia na Sayansi
  • Sekretarieti ya Ajira

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mpwapwa - Dodoma, Tanzania

    Anwani: S.L.P 12

    Simu: 255 26 2320122/2320

    Simu ya Kiganjani: 0684705551

    Barua pepe: info@mpwapwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovutii

Copyright © 2021 Mpwapwa District Council . All rights reserved.