Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Ndg Gideon Bakuza ameongozana na wakuu wa idara na vitengo leo Febuari 2,2026 wametembelea eneo linaloendelea kujengwa Ofisi Mpya ya Halmashauri kwa lengo la kufanya kikao cha makubaliano ya muendelezo wa mradi huo kwa hatua ya pili na kukagua mradi kwa hatua ya kwanzo iliyomalizika.
Wakati wa kikao hicho Ndg Bakuza amemtaka Mkandarasi wa Mradi wa Jengo la Halmashauri kuhakikisha wanaenda na muda wa makubaliano ambao ni siku 120 kwa maana ya miezi minne na ikiwezekana iwe chini ya hapo ili kuweza kukimbizana na fedha za mradi huo,pia amewasisitiza uwepo wa wataalamu wote wanahusika na ujenzi,vifaa pamoja na kuengeza juhudi na maarifa ambayo yatasaidia katika kuifanya kazi hiyo kwa urahisi.
Mradi wa Jengo jipya la Halmashauri ya Mpwapwa unatekelezwa katika Kata ya Mpwapwa Mjini,kijiji cha Ilolo
Mradi wa Jengo hilo kwa hatua ya mwanzo limegharimu kiasi cha Shiling 800,000,000 kutoka Serikali kuu.








Mpwapwa - Dodoma, Tanzania
Anwani: S.L.P 12
Simu: 255 26 2320122/2320
Simu ya Kiganjani: 0684705551
Barua pepe: info@mpwapwadc.go.tz
Copyright © 2021 Mpwapwa District Council . All rights reserved.