• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mpwapwa District Council
Mpwapwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
        • Fedha
        • Biashara
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Mali asili
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Usafi na Mazingira
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Habari Mawasiliano na Tehama
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Nyuki
    • Mamlaka
      • Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mpwapwa
      • Mamlaka ya Maji Mpwapwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashuri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa mbali mbali
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo mbali mbali
    • Simulizi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video mbali mbali
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Wakulima Wahimizwa Kuandaa Mashamba Mapema

Posted on: November 29th, 2018

(Na: Shaibu J. Masasi, Afisa TEHAMA - Mpwapwa)

Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa leo amefanya ziara katika kata ya Lupeta na Mpwapwa Mjini kwa ajili ya kukagua shughuli za utayarishwaji wa mashamba katika msimu huu wa kilimo, na amekutana na wakulima wa maeneo hayo. Katika hotuba yake kwa wananchi wa maeneo hayo Mkuu wa Wilaya amewahimiza na kuwakumbusha wakulima kuwa msimu wa kilimo unakaribia hivyo kila mwananchi aanze kuandaa mashamba. Pia amesisitiza kuwa kila kijana mwenye uwezo wa kufanyakazi awe na shamba la mzao ya chakula na mazao ya biashara hasa zao la korosho.

Mkuu wa Wilaya Mhe. Jabir Shekimweri akiuchunguza mche wa mkorosho ukiwa umeanza kutoa maua, hii ni baadhi ya miche ya kisasa iliyopandwa mwaka 2017 katika shamba la mkulima mmoja kata ya Lupeta 

Aidha Mkuu wa Wilaya amewaagiza maafisa Kilimo wa Kata kuhakikisha wanawasaidia wakulima kwa kuwapa maelekezo ya kitaalamu Katika upandaji na usimamizi wa zao la korosho ili liwe na tija kwa wakulima hao.

Mhe. Shekimweri ametoa maagizo hayo Jana Katika ziara ya ukaguzi wa mashamba ya korosho na uandaji wa viriba vya mbegu za korosho unaoandaliwa na kikundi cha akina Mama Wilunze kwa msimu wa kilimo wa mwaka 2018/2019. Pia amesema Katika msimu wa kilimo wa mwaka 2017/2018 aliiagiza kila kijiji kuwa na shamba darasa la korosho jambo alilosema bado halijatekelezwa kwa vijiji vingi vya Mpwapwa na awataka mwaka huu kutekeleza.

Aidha Shekimweri amewaomba madiwani na viongozi wote wa kuteuliwa na kuchaguliwa kuihimiza jamii juu ya mabadiliko ya Mpwapwa mpya inayolenga katika mabadiliko ya kiuchumi kwa kuwa na zao mkakati la Wilaya linalo lenga kuinua uchumi pamoja na uboreshaji wa huduma za jamii ikiwemo Elimu, afya na huduma za maji.

Mkuu wa Wilaya Mhe. Jabir Shekimweri (katikati) akiwa na Afisa Kilimo wilaya Bi. Maria Leshalu (kulia) wakikagua mashamba yaliyotayarishwa na wakulima katika msimu huu wa kilimo  kata ya Lupeta

Kwa upande wake Afisa Kilimo wa Wilaya hiyo Bi. Maria Leshalu amesema kama zao la korosho likatikiwa mkazo na kufuatiliwa kwa kanuni za kilimo, basi jamii ya Mpwapwa ndani ya miaka mitano ijayo itaimarika kiuchumi na kimazingira. Amesema wananchi lazima wafuate maelekezo ya wataalamu ili kuweza kupata tija katika zao hili.Pia Afisa Kilimo huyo amewataka wananchi kuweza kuzingatia taarifa za hali ya hewa ili kuweza kuandaa mashamba yao kwa msimu wa kilimo kwa mwaka 2018/2019. 

Mkuu wa Wilaya Mhe. Jabir Shekimweri (kushoto) akikagua kitaru cha miche ya mikorosho ikiwa katika viriba kama maandalizi ya wakulima katika msimu huu wa kilimo eneo la Mji Mpya kata ya Mpwapwa Mjini 

Mmoja wa wananchi ambao ni wakulima wa korosho amesema upatikaji wa dawa za kupiga katika zao hilo kunatishia uzalishaji kupungua na baadhi ya miche kunyauka. Kutokana na changamoto hiyo, Afisa Kilimo wa Wilaya ameahidi kuishughulikia mara moja hasa katika upatikanaji wa dawa za kuua wadudu na kutibu magonjwa ya korosho.

Na: Shaibu J. Masasi, Afisa TEHAMA - Mpwapwa

Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye usahili MpwapwaDC June 27, 2022
  • Tangazo la nafasi za kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa. 2022 April 20, 2022
  • Tangazo la Nafasi za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa May 2022 May 31, 2022
  • Tangazo la kuahirishwa kwa Usahili Halmashauri ya Mpwapwa June 22, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • NORISH NA WAKULIMA WILAYA YA MPWAPWA

    May 06, 2025
  • VIONGOZI KUTOKA OFISI YA MAKAMU WA RAIS ZANZIBAR WATEMBELEA MIRADI YA MFUKO WA JIMBO MPWAPWA

    May 09, 2025
  • FUM YAFANYA ZIARA MIRADI YA KIMAENDELEO

    April 29, 2025
  • MAADHIMISHO YA MEI MOSI YAFANYIKA SINGIDA

    May 01, 2025
  • Tazama zote

Video

Video ya Mpango wa Uuzaji wa Viwanja Eneo la Mazae Block "E" katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa -2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa
  • Muundo wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani
  • Ratiba ya Vikao vya Madiwani

Viunganishi Linganishi

  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Wizara ya Fedha na Mipango
  • Utumishi portal
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu Teknolojia na Sayansi
  • Sekretarieti ya Ajira

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mpwapwa - Dodoma, Tanzania

    Anwani: S.L.P 12

    Simu: 255 26 2320122/2320

    Simu ya Kiganjani: 0684705551

    Barua pepe: info@mpwapwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovutii

Copyright © 2021 Mpwapwa District Council . All rights reserved.