• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mpwapwa District Council
Mpwapwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
        • Fedha
        • Biashara
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Mali asili
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Usafi na Mazingira
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Habari Mawasiliano na Tehama
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Nyuki
    • Mamlaka
      • Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mpwapwa
      • Mamlaka ya Maji Mpwapwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashuri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa mbali mbali
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo mbali mbali
    • Simulizi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video mbali mbali
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Viongozi wa Tarafa ya Mpwapwa Wapatiwa Mikakati Dhidi ya Corona

Posted on: March 26th, 2020

Na: Shaibu J. Masasi; Afisa TEHAMA - Mpwapwa Dc

Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Jabir Mussa Shekimweri amekutana na viongozi wote wa tarafa ya Mpwapwa ili kuwapatia Mikakati ya Wilaya ya kupambana na Ugonjwa Hatari wa Corona (COVID-19) unaosambaa kwa kasi katika Nchi nyingi duniani, ambapo kwa sasa Nchi ya Tanzania imethibika kuwa na wagonjwa 12.

Katika Mkutano huo uliofanyika katika Ukumbi wa Mkuu wa Wilaya Umehudhuriwa na Kamati ya Ulinzi na Usala ya Wilaya,  Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa Mhe. George Fuime ambaye pia ni Diwani wa kata ya Mpwapwa Mjini, Ndugu. Paul M. Sweya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa, Wataalam toka Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa, Katibu Tarafa ya Mpwapwa, Watendaji wa Kata wote, Wenyeviti wa vijiji na Wenyeviti wa Vitongoji.

Aidha viongozi hao wamepatiwa elimu sahihi ya corona kuanzia maana ya ugonjwa wa Corona-19, unavyosambaa au kuambukizwa, dalili zake, jinsi ya kujikinga na namna ya kupata msaada ya matibabu iliyotolewa na Daktari Kikoti Jumaa Morijo toka Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa. Pia viongozi waliohudhuria Kikao hicho wamepewa vipeperushi vilivyotengenezwa na Wizara ya Afya, Maendelo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kushirikiana na Shirika la Msalama Mwekundu (RED CROSS) ili kuwawezesha wananchi kufahamu mambo ya msingi katika kujilinda na ugonjwa huu wa corona. Katika vipeperushi hivyo kumeelezwa maana ya corona-19, jinsi ungonjwa unavyoosambaa, dalili za corona, jinsi ya kijilinda na jinsi ya kupata msaada wa matibabu.

Kipeperushi Kuhusu Ugonjwa wa Homa kali ya Mapafu Unaosababishwa na Virusi vya CoronaDaktari Kikoti wa Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa ambaye pia ni Moja kati ya Waelimishaji toka katika Timu ya Wilaya ya Waelimushaji Juu ya Corona

Katika kikao hicho viongozi wa tarafa ya Mpwapwa wameelimishwa juu wa Ugonjwa wa COVID-19 na kupewa fursa ya kuuliza maswali na maswali yote yamejibiwa vizuri na hivyo kuimarisha uelewa wa washiriki hao. Pia viongozi hao wameahidi kwa kushirikiana na wataalam wa Afya na wajumbe wa Timu ya Wilaya ya Udhibiti dhidi Corona kwenda kutoa elimu hii kwa wananchi wanaowaongoza.

Baada ya Viongozi hao kujengewa uelewa juu ya Ungonjwa wa Corona, Mkuu wa Wilaya Mhe. Shekimweri alipokeza usikivu mzuri uliofanywa na viongozi hao waliohudhuria kikao hicho na kuuliza masawali ya msingi yenye kutaka kuelewa vizuri ugonjwa huu. Pia amempongeza Daktari Kikoti kwa kusema "Daktari umetoa mafunzo mazuri kwa kutumia lugha nyepese ya kiswahili ambapo kila mmoja ameelewa".

Aidha Mkuu wa Wilaya amewataka viongozi na wananchi kuondoa hofu ila kuchukua tahadhari dhidi ya corona, kufanya kazi kwa bidii, kuepuka mikusanyiko isiyo yalazima, kuacha safari zisizo za lazima na kukaa umbali wa mita moja toka mtu mmoja hadi mwingine kila tunapokaa na kunawa mikono kwa maji safi yanayotiririka na sabuni mara kwa mara. 

Mkuu wa Wilaya amesema kwamba "Wilaya ya Mpwapwa imejipanga kikamilifu katika kupambana na kuenea kwa ugonjwa wa corona kwa kuunda kamati 5 za kuelimisha juu ya corona, kuweka mikakati ya Kila taasisi kuweka ndoo ya maji yanayotiririka na sabuni na kufanya vikao na watumishi. Pia ameongeza kuwa "Wilaya imetenga Logde ya Chichi, Ark hotel na Kalunguyeye zitapokea washukiwa wa ugonjwa wa corona-19 waliosafiri toka nje ya nchi na watajigharimia wenyewe kwa siku 14". 

Vilevile Mkuu wa Wilaya amesema kuwa "Kama kukitokea wagonjwa  wa corona katika Wilaya yetu, kila zahanati na vituo vya afya vimetengwa vyumba kwa ajili ya kuwapokea wagonjwa wanaohisiwa kuwa na  corona na kupatiwa matibabu ya dalili watakaoonyesha wakati majibu ya vipimo yanasubiriwa, tumetenga maeneo ya kuwahifadhi washukiwa wa ugonjwa wa corona kama watabainika katika wilaya yetu katika Chuo cha Ualimu Mpwapwa, Chuo cha Mifugo ( LITA), Taasisi ya Utafiti wa Mifugo (TALIRI), na zahanati ya Mazae kwa ajili ya kulazwa wagonjwa wa corona ".

Mwisho Mkuu wa Wilaya amewashukuru viongozi kwa kukubali wito wake na kutapa mafunzo ya corona na hivyo anatumaini watakuwa mabalozi wazuri kwa wananchi.

******Mwisho****


Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye usahili MpwapwaDC June 27, 2022
  • Tangazo la nafasi za kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa. 2022 April 20, 2022
  • Tangazo la Nafasi za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa May 2022 May 31, 2022
  • Tangazo la kuahirishwa kwa Usahili Halmashauri ya Mpwapwa June 22, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • NORISH NA WAKULIMA WILAYA YA MPWAPWA

    May 06, 2025
  • VIONGOZI KUTOKA OFISI YA MAKAMU WA RAIS ZANZIBAR WATEMBELEA MIRADI YA MFUKO WA JIMBO MPWAPWA

    May 09, 2025
  • FUM YAFANYA ZIARA MIRADI YA KIMAENDELEO

    April 29, 2025
  • MAADHIMISHO YA MEI MOSI YAFANYIKA SINGIDA

    May 01, 2025
  • Tazama zote

Video

Video ya Mpango wa Uuzaji wa Viwanja Eneo la Mazae Block "E" katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa -2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa
  • Muundo wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani
  • Ratiba ya Vikao vya Madiwani

Viunganishi Linganishi

  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Wizara ya Fedha na Mipango
  • Utumishi portal
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu Teknolojia na Sayansi
  • Sekretarieti ya Ajira

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mpwapwa - Dodoma, Tanzania

    Anwani: S.L.P 12

    Simu: 255 26 2320122/2320

    Simu ya Kiganjani: 0684705551

    Barua pepe: info@mpwapwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovutii

Copyright © 2021 Mpwapwa District Council . All rights reserved.