• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mpwapwa District Council
Mpwapwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
        • Fedha
        • Biashara
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Mali asili
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Usafi na Mazingira
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Habari Mawasiliano na Tehama
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Nyuki
    • Mamlaka
      • Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mpwapwa
      • Mamlaka ya Maji Mpwapwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashuri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa mbali mbali
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo mbali mbali
    • Simulizi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video mbali mbali
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Siku ya Unyonyeshaji Yafana, Mkuu wa Wilaya Atoa Zawadi kwa Wazazi

Posted on: August 7th, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa ambaye ndiye mgeni rasmi, Mhe. Jabir Shekimweni amefungua maadhimisho ya Siku ya Unyonyeshaji Dunia yaliyofanyika kiwilaya katika ukumbi wa kliniki ya watoto katika Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa. Maadhimisho haya yamehudhuriwa na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa Mhe. George Fuime, madaktari, wauguzi, wataalamu wengine, wazazi, wajawazito na wananchi kwa ujumla. 

Siku ya Unyonyeshaji Duniani huadhimishwa kuanzia tarehe 1 Agosti mpaka 7 Agosti kila mwaka ambapo kwa mwaka huu kauli mbiu ni “UNYONYESHAJI WA, MAZIWA YA MAMA NI MSINGI WA MAISHA YA MTOTO”. 

 Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Jabir Shekimweri (aliyesimama) Akitoa Hotuba katika Siku ya Unyenyeshaji Dunia. (Picha na: Shaibu J. Masasi, Afisa TEHAMA - Mpwapwa)

Pia maadhimisho haya yameambatana na mafunzo ya jinsi ya kumnyonyesha mtoto toka anapozaliwa hadi kufika umri wa miaka miwili. Akitoa mafunzo haya Bi.Petronida Mahanyila ambaye ni Mratibu wa Afya ya Mama na Mtoto amesema "Mtoto anapozaliwa anatakiwa kunyonyeshwa kwa muda wa miezi sita mfululizo bila kumlisha vyakula vingine, na baada ya miezi sita anatakiwa kuendeleakukunyonyeshwa kwa muda wa miaka miwili sawa na siku 1000 huku akichanganyiwa vyakula laini kama vile uji wa nafaka wenye virutubisho muhimu kwa ukuaji wa mtoto, juisi za matunda na vyakula vingine vilivyosagwa na kuwa laini".

Vile vile ameongeza kuwa "mama mjamzito anapaswa kuhudhuria kliniki mara tu anapata mimba ili aweze kupatiwa kinga mbalimbali za kumlinda mtoto aliyetumboni tangu mama anapopata ujauzito hadi kujifungua, kinga hizo zinasaidia kuongeza damu ya mama, kuzuia mtoto kuzaliwa akiwa na kasoro kama za mgongo wazi, mdomo kuchanika, kutopata maambukizi toka kwa mama, kumlinda mama na magonjwa mbalimbali"

Bi.Petronida Mahanyila ambaye ni Mratibu wa Afya ya Mama na Mtoto (aliyesimama) Akitoa Mafunzo ya Unyonyeshaji wa Mtoto na lishe bora kwa Mama na Mtoto katika Siku ya Unyenyeshaji Dunia. (Picha na: Shaibu J. Masasi, Afisa TEHAMA - Mpwapwa)

Katika hotuba yake mgeni rasmi amewaasa wajawazito kujifungulia hospitalini na sio kujifungulia nyumbani kwa kuwa kujifungulia hospitalini mama na mtoto anakuwa katika ungalizi salama kwa kupata matibabu  na ushauri wa ukuaji wa mtoto. Pia ameongeza kuwa wazazi wanatakiwa kuwanyonyesha watoto wao kwa kuwa maziwa ya mama yana virutumisho vyote ambavyo vinamjenga mtoto kiakili na hivyo kupata watoto wenye akili nzuri na afya bora.

Pia ameeleza kuwa kumnyonyesha mtoto kwa muda wa miaka miwili kunasaidia kupunguza uwezekana wa kupata saratani ya matiti kwa kuwa maziwa yafanya mrundikano wa katika matiti na mwisho wa siku mama anweza akapata saratani ya matiti.

Vile vile amesisitiza kuwa wazazi watumie uzazi wa mpango ili kupata watoto kwa wakati na kwa nafasi hii inasaidia kupata watoto wenye afya bora na  wazazi kuweza kuwapatia mahitaji muhimu.

Wazazi wakisikiliza kwa Umakini Hotuba ya Mgeni Rasmi Ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Jabir Shekimweri katika Siku ya Unyenyeshaji Dunia. (Picha na: Shaibu J. Masasi, Afisa TEHAMA - Mpwapwa)

Baada ya kutoa hotuba hiyo Mgeni rasmi ametoa zawadi ya sabuni ya unga yenye ujazo wa kilogram moja kwa kila mzazi na mjamzito. Hivyo wazazi wamempongeza sana Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Jabir Shekimweri kwa msaada huo na nasaa zake, na wameahidi kutekeleza mambo yote ya muhimu katika ukuaji wa watoto wao.

Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Jabir Shekimweri (aliyesimama) Akitoa Zawadi ya Sabuni ya Unga Kilogram Moja kwa Kila Mama Mjamzito na Mzazi katika Siku ya Unyenyeshaji Dunia. (Picha na: Shaibu J. Masasi, Afisa TEHAMA - Mpwapwa)

Kwa taarifa zaidi juu ya taarifa Hii pakua Nyaraka hii hapa chini:

Risala kwa Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa katika Siku ya Unyonyeshaji Duniani.pdf

Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye usahili MpwapwaDC June 27, 2022
  • Tangazo la nafasi za kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa. 2022 April 20, 2022
  • Tangazo la Nafasi za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa May 2022 May 31, 2022
  • Tangazo la kuahirishwa kwa Usahili Halmashauri ya Mpwapwa June 22, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • NORISH NA WAKULIMA WILAYA YA MPWAPWA

    May 06, 2025
  • VIONGOZI KUTOKA OFISI YA MAKAMU WA RAIS ZANZIBAR WATEMBELEA MIRADI YA MFUKO WA JIMBO MPWAPWA

    May 09, 2025
  • FUM YAFANYA ZIARA MIRADI YA KIMAENDELEO

    April 29, 2025
  • MAADHIMISHO YA MEI MOSI YAFANYIKA SINGIDA

    May 01, 2025
  • Tazama zote

Video

Video ya Mpango wa Uuzaji wa Viwanja Eneo la Mazae Block "E" katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa -2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa
  • Muundo wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani
  • Ratiba ya Vikao vya Madiwani

Viunganishi Linganishi

  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Wizara ya Fedha na Mipango
  • Utumishi portal
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu Teknolojia na Sayansi
  • Sekretarieti ya Ajira

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mpwapwa - Dodoma, Tanzania

    Anwani: S.L.P 12

    Simu: 255 26 2320122/2320

    Simu ya Kiganjani: 0684705551

    Barua pepe: info@mpwapwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovutii

Copyright © 2021 Mpwapwa District Council . All rights reserved.