• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mpwapwa District Council
Mpwapwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
        • Fedha
        • Biashara
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Mali asili
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Usafi na Mazingira
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Habari Mawasiliano na Tehama
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Nyuki
    • Mamlaka
      • Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mpwapwa
      • Mamlaka ya Maji Mpwapwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashuri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa mbali mbali
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo mbali mbali
    • Simulizi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video mbali mbali
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Program ya Kuwakinga Wasichana Waliobalehe Yatambulishwa Mpwapwa

Posted on: June 12th, 2018

Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kushirikiana na Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS), Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), Shirika la AM-FM na Asasi ya Kiraia Tanzania Youth Alliance (TAYOA) leo imetambulisha program maalam ya kuwakinga wasichana waliobalehe na wanawake vijana ndani na nje ya shule katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa. Katika warsha hii ya siku moja  imefanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa na imehudhuriwa na wadau mbalimbali wakiwemo waheshimiwa madiwani ambao ni wenye viti wa kamati za kudumu za Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa, wakuu wa idara za afya, elimu, maendeleo ya jamii, mipango na takwimu, viongozi wa dini na Asasi za Kiraia. Aidha warsha hii imefunguliwa na Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya ya Mpwapwa Ndg. Apolonia Temu akimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Jabir Mussa Shekimweri na kufungwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma za Jamii Mhe. Joctan Cheligah ambaye ni diwani wa kata ya Lumuma akimwakilisha Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Donath Nghwenzi ambaye pia ni diwani wa kata ya Massa. Pia warsha hii imehudhuriwa na Ndg. Khamlo Njovu ambaye ni Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto akimwakilisha Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashuri ya Mpwapwa Ndg. Maria Leshalu.

Wakuu wa idara, waheshimiwa madiwani na wadau wengine wakifuatilia warsha ya kuwakinga wasichana (kulia mbele ni Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Dkt. Said Mawji). ( Picha na Dkt. Said Mawji, Mganga Mkuu - Wilaya ya Mpwapwa).

Program hii ni ya majaribio na itatekelezwa kwa muda wa miaka mitatu katika mikoa mitatu tu Tanzania Bara, mikoa hiyo ni Singida, Morogoro na Dodoma. Pia itashirisha halmashauri za wilaya kumi (10) za miko hiyo ambapo kwa mkoa wa Dodoma wilaya za Mpwapwa, Bahi, kongwa na Kondoa zimeteuliwa kwenye program hii.

Mhe. Joctan Cheligah (katikati) akifunga warsha hiyo, (kulia) Ndg. Khamlo Njovu, mkuu wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na (kushoto) Ndg. Emmanuel mkuu wa msafara toka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.(Picha na: Dkt. Said Mawji - Mganga Mkuu Wilaya ya Mpwapwa)

Mtaalam toka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ndg. Emmanuel,  amesema kuwa program hii inawalenga hasa wasichana wenye umri wa miaka 10 hadi 24 walioko kwenye mpango wa kaya masikini katika vijiji 57 vilivyopo wilaya ya Mpwapwa. Lengo likiwa ni kuwawezesha kujitambua, kujikinga na mihemko inayosababishwa na mabadiliko ya mwili katika ukuaji.

Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye usahili MpwapwaDC June 27, 2022
  • Tangazo la nafasi za kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa. 2022 April 20, 2022
  • Tangazo la Nafasi za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa May 2022 May 31, 2022
  • Tangazo la kuahirishwa kwa Usahili Halmashauri ya Mpwapwa June 22, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • NORISH NA WAKULIMA WILAYA YA MPWAPWA

    May 06, 2025
  • VIONGOZI KUTOKA OFISI YA MAKAMU WA RAIS ZANZIBAR WATEMBELEA MIRADI YA MFUKO WA JIMBO MPWAPWA

    May 09, 2025
  • FUM YAFANYA ZIARA MIRADI YA KIMAENDELEO

    April 29, 2025
  • MAADHIMISHO YA MEI MOSI YAFANYIKA SINGIDA

    May 01, 2025
  • Tazama zote

Video

Video ya Mpango wa Uuzaji wa Viwanja Eneo la Mazae Block "E" katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa -2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa
  • Muundo wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani
  • Ratiba ya Vikao vya Madiwani

Viunganishi Linganishi

  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Wizara ya Fedha na Mipango
  • Utumishi portal
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu Teknolojia na Sayansi
  • Sekretarieti ya Ajira

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mpwapwa - Dodoma, Tanzania

    Anwani: S.L.P 12

    Simu: 255 26 2320122/2320

    Simu ya Kiganjani: 0684705551

    Barua pepe: info@mpwapwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovutii

Copyright © 2021 Mpwapwa District Council . All rights reserved.