• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mpwapwa District Council
Mpwapwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
        • Fedha
        • Biashara
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Mali asili
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Usafi na Mazingira
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Habari Mawasiliano na Tehama
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Nyuki
    • Mamlaka
      • Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mpwapwa
      • Mamlaka ya Maji Mpwapwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashuri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa mbali mbali
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo mbali mbali
    • Simulizi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video mbali mbali
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Mwenge wa Uhuru 2019 Waingia Mpwapwa

Posted on: August 12th, 2019

(Na: Shaibu J. Masasi, Afisa TEHAMA - Mpwapwa)

Mwenge wa Uhuru 2019 umeingia Wilaya ya Mpwapwa na kukembelea, Kuweka mawe ya msingi na kuzindua miradi mitano yenye thamani ya Tsh. 711,733,640.89 Miradi hiyo ni Mradi wa Ufugaji nyuki uliopo kwa Mshango kata ya Vinghawe, mradi wa Wodi ya matibabu ya Utapiamlo mkali iliyopo katika Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa kata ya Mpwapwa Mjini yenye thamani ya Tsh 130,480,586.00, mradi wa Mnada wa kisasa wa Ilolo uliopo kata ya Mpwapwa Mjini, mradi wa Maji Mzase uliopo kata ya Berege na mradi wa Maktaba ya Shule ya Sekondari Kibakwe iliyopo kata ya Kibakwe.

Mwenye wa Uhuru 2019 unaoongozwa na Mkimbiza Mwenge Kitaifa Ndugu. Mzee Mkongea Ali amekubali kuweka jiwe la msingi katika jengo la wodi ya utapiamlo mkali japo kuna maelekezo ya marekebisho machache ameyatoka ili yafanyiwekazi kama kutenganisha chemba ya maji ya bafuni na kunawa mikoni yanatoka katika masinki ya kunawia.

Pia amekubali kutembelea mradi wa ufugaji nyuki na kugawa mizinga ya nyuki 28 kwa vikundi vya ufugaji nyuki kwa Mshango katika kata ya Vinghawe. "Nawagawai mizinga hii kweli mfanyekazi ya ufugaji nyuki na kutunza mazingira ya sehemu hii hasa upanda wa miti, uhifadhi wa vyanzo vya maji na kutochoma moto ovyo" amesema Ndugu. Ali. 

Naye Waziri wa Nchi, ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. George Simbachawe amepata fursa ya kuongea na wananchi wa Mpwapwa juu ya utunzaji wa mazingira kwa kuwataka wananchi wa wilaya ya Mpwapwa kupanda miti maji, kutunza vyanzo vya maji, kutochoma moto misitu, kutochungia na kulima katika vyanzo vya maji na kufuga nyuki ili kujipatia kipato mmbadala. Pia amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Jabir Shekimweri kusimamia zoezi la uwekwaji alama katika maeneo yatakayozuiawa wananchi kufanya shughuli za kibinadamu hasa katika vyanzo vya maji kwa sheria ya kutofanya shughuli za kibinadamu mita 60 toka katika chanzo.

Aidha Mwenge wa Uhuru 2019 umezindua Miundombinu ya Mnada wa Ilolo ambao ni mnada wa kisasa kwa wilaya ya Mpwapwa wenye mazizi mawili makubwa ya mbuzi na ng'ombe, machinjio ya kisasa, ofisi za wakusanya ushuru na wasimamizi wa mnada na pakilio la ng'ombe. Ndugu. Mzee Mkongea Ali amekubali kuzindua miundombinu hii japo ametoa maelekezo machache ya kuboresha ofisi za wasimamizi wa mnada kwa kuwa hazi madirisha ya vioo ili kuzuia vumbi na mvua kuweza kuingia.

Vile vile Mwenge wa Uhuru 2019 umetembelea Mradi wa maji Mzase ambao umekataliwa kuzinduliwa kwa kuwa upo chini ya kiwango kwa mujibu wa Mkimbiza Mwenge kitaifa Ndugu. Ali, amesema "Mradi huu wa maji haujakidhi vigezo kama nondo na matofali hakupelekwa maabara kupimwa, ulizio uliozungushiwa katika kisima na tanki la maji sio ulioonyeshwa katika BOQ" hivyo mradi huu hautazinduliwa na mwenge wa Uhuru 2019, amesisitiza. Badala yake ameruhusu wananchi kutomia maji hayo ni safi na salama kwa matumizi ya binadamu. Pia kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge 2019 kitaifa amemuogiza Mkuu wa TAKUKURU Wilaya ya Mpwapwa Bi. Juliet Mtuyi kuchunguza mradi wa maji Mzase na taarifa ipelekwe TAKUKURU makao makuu na yeye apate nakala popote alipo.

Mwisho, Mwenge wa Uhuru 2019 umezindua maktaba ya kisasa katika shule ya sekondari Kibakwe japo ametoa maelekezo machache ikiwemo kuogeza viti, meza na vitabu ili wanafunzi waweze kupata fursa nzuri ya kujisomea.


Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye usahili MpwapwaDC June 27, 2022
  • Tangazo la nafasi za kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa. 2022 April 20, 2022
  • Tangazo la Nafasi za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa May 2022 May 31, 2022
  • Tangazo la kuahirishwa kwa Usahili Halmashauri ya Mpwapwa June 22, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • NORISH NA WAKULIMA WILAYA YA MPWAPWA

    May 06, 2025
  • VIONGOZI KUTOKA OFISI YA MAKAMU WA RAIS ZANZIBAR WATEMBELEA MIRADI YA MFUKO WA JIMBO MPWAPWA

    May 09, 2025
  • FUM YAFANYA ZIARA MIRADI YA KIMAENDELEO

    April 29, 2025
  • MAADHIMISHO YA MEI MOSI YAFANYIKA SINGIDA

    May 01, 2025
  • Tazama zote

Video

Video ya Mpango wa Uuzaji wa Viwanja Eneo la Mazae Block "E" katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa -2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa
  • Muundo wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani
  • Ratiba ya Vikao vya Madiwani

Viunganishi Linganishi

  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Wizara ya Fedha na Mipango
  • Utumishi portal
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu Teknolojia na Sayansi
  • Sekretarieti ya Ajira

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mpwapwa - Dodoma, Tanzania

    Anwani: S.L.P 12

    Simu: 255 26 2320122/2320

    Simu ya Kiganjani: 0684705551

    Barua pepe: info@mpwapwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovutii

Copyright © 2021 Mpwapwa District Council . All rights reserved.