• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mpwapwa District Council
Mpwapwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
        • Fedha
        • Biashara
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Mali asili
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Usafi na Mazingira
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Habari Mawasiliano na Tehama
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Nyuki
    • Mamlaka
      • Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mpwapwa
      • Mamlaka ya Maji Mpwapwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashuri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa mbali mbali
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo mbali mbali
    • Simulizi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video mbali mbali
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Mpwapwa Yawa Mfano wa Kuigwa kwa Halmashauri Zote za Dodoma

Posted on: March 6th, 2019

(Na: Shaibu J. Masasi, Afisa TEHAMA - Mpwapwa)

Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa imetajwa kuwa ni moja wapo ya Halmashauri inayofanya vizuri katika mambo mbalimbali kama vile Utawala, usimamizi wa miradi na Ukusanyaji wa Mapato. Kauli hiyo imetolewa na Katibu Tawala Msaidizi Menejimenti ya Serikali za Mitaa Ndugu. Emmanuel Kuboja katika Kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa tarehe 06/03/2019.  

Katibu Tawala Masaidizi menejimenti ya serikali za Mitaa Ndug. Emmanuel Kuboja (wa kwanza kushoto aliyesimama), Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa Ndug. Paul Mamba Sweya (wa pili kushoto), Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Donath S. Nghwenzi (wa pili kulia) na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa Mhe. George Fuime (wa kwanza kulia) wakiwa katika Kikao cha Baraza la Madiwani.

"Mkuu wa Mkoa pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Dodoma ina  imani kubwa na  uongozi wa sasa wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa kwa kuwa mapato kwa sasa yameimarika na kwa takwimu nilizonazo mpaka sasa mmekusanya  mapato ya ndani kwa asilimia 74.26 " amesema Ndugu. Kuboja.  Pia amemshukuru Mwenyekiti wa Halmasahuri ya Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Donath S. Nghwezi kwa kuendesha baraza la madiwani kwa umairi mkubwa. Vile vile Ndugu Kuboja ameeleza kuwa Mpwapwa inaweza kuwa Mamlaka ya Mji au Manispaa moja kwa moja kama ukusanyaji wa mapato na mikakati mizuri mliyoweka itaendelea hivi hivi.

Ndugu Kuboja ameongeza kuwa katika bajeti ya mwaka huu 2019/2020 mnatakiwa kuzingatia vipaumbele vya Kitaifa, Kimkoa na Kiwilaya, kwanza; kuweka juhudi katika Elimu hasa katika kujenga madarasa  na kuongeza juhudi ili kuhakikisha ufaulu unaongezeka. pili, kuweka mikakati kuhamasisha ukusanyaji wa mapato ya ndani kwa kuwa wafadhiri na fedha toka  Serikali Kuu zimepunguzwa. Pia ameongeza kama kuna mtu atakaye haribu utaratibu huu mzuri mlioweka wa kukusanya napato hatua kali zikuliwe dhidi yake.

Waheshimiwa madiwani, wakuu wa idara na wageni waalikwa wakiwa katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa kwenye Kikao cha Baraza la Madiwani.

Aidha, Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Jabir Shekimweri amewaeleza Waheshimiwa Madiwani kuwa kwa sasa mapato ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa yameongeza na kasi ya ukusanyaji wa mapato imeimarika, kwa taarifa iliyopo mpaka mwisho wa mwezi huu wa Februari mapato yamekusanywa na kufikia asilimia 85 ambayo bado hayajatumwa katika mfumo ndio maana katika mfumo bado kuna taarifa ya asilimia 74.26. Mwaka jana 2018 mwezi kama huu kulikuw na asilimia 26 tu ya makusanyo ya mapato ya ndani ndio maana tulichukua hatua zile na nyote mlishuhudia , amesema Mhe. Shekimweri. Kwa sasa inaonyesha kuwa kuna jitihada zinafanyika katika kukusanya mapato.

 Pia Mhe. Kimweri amewataka wataalam na waheshimiwa madiwani kufuata sheria, kanuni na taratibu katika kufanya kazi za umma. "Wito wangu kila mmoja wenu afuate Sheria, Kanuni na Taratibu, mashinikizo yoyote hayatawaweka salama".

Mwisho Mkuu wa Wilaya amemtaka Afisa Utumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa Ndugu Pius Sayayi kuwaelekeza watumishi sheria, kanuni na taratibu kupitia baraza la watumishi na hasa watumishi wapya.



Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye usahili MpwapwaDC June 27, 2022
  • Tangazo la nafasi za kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa. 2022 April 20, 2022
  • Tangazo la Nafasi za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa May 2022 May 31, 2022
  • Tangazo la kuahirishwa kwa Usahili Halmashauri ya Mpwapwa June 22, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • NORISH NA WAKULIMA WILAYA YA MPWAPWA

    May 06, 2025
  • VIONGOZI KUTOKA OFISI YA MAKAMU WA RAIS ZANZIBAR WATEMBELEA MIRADI YA MFUKO WA JIMBO MPWAPWA

    May 09, 2025
  • FUM YAFANYA ZIARA MIRADI YA KIMAENDELEO

    April 29, 2025
  • MAADHIMISHO YA MEI MOSI YAFANYIKA SINGIDA

    May 01, 2025
  • Tazama zote

Video

Video ya Mpango wa Uuzaji wa Viwanja Eneo la Mazae Block "E" katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa -2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa
  • Muundo wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani
  • Ratiba ya Vikao vya Madiwani

Viunganishi Linganishi

  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Wizara ya Fedha na Mipango
  • Utumishi portal
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu Teknolojia na Sayansi
  • Sekretarieti ya Ajira

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mpwapwa - Dodoma, Tanzania

    Anwani: S.L.P 12

    Simu: 255 26 2320122/2320

    Simu ya Kiganjani: 0684705551

    Barua pepe: info@mpwapwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovutii

Copyright © 2021 Mpwapwa District Council . All rights reserved.