• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mpwapwa District Council
Mpwapwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
        • Fedha
        • Biashara
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Mali asili
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Usafi na Mazingira
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Habari Mawasiliano na Tehama
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Nyuki
    • Mamlaka
      • Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mpwapwa
      • Mamlaka ya Maji Mpwapwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashuri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa mbali mbali
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo mbali mbali
    • Simulizi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video mbali mbali
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Mpwapwa Yaadhimisha Siku ya Mashujaa kwa Kufanya Usafi Maradufu

Posted on: July 25th, 2018

Maadhimisho ya Siku ya Mashujaa hufanyika kila mwaka tarehe 25 Julai kama moja wapo ya kuwakumbuka na kuwaenzi mashujaa waliojitolea kwa moyo wa uzalendo kupigana vita vya ukombozi ili kuikomboa Nchi ya Tanzania katika mikono mwa wakoloni na watu wenye hira na tamaa ya kutaka kuitawala kimabavu. 

Kwa mwaka huu wa 2018 siku hii ya mashujaa imeazimishwa kiwilaya hapa Mpwapwa kwa kufanya usafi katika maeneo muhimu ikiwemo Soko Kuu la Mjini Mpwapwa na Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa ambapo wananchi kwa ujumla wamejitokeza kwa wingi ili kushsiriki katika usafi huo. Pia baada ya zoezi la usafi kukamilika katika maeneo yote ilifuatiawa na zoezi la UCHANGIAJI DAMU kwa hiari, ambapo wadau walijitokea kufanikisha hili.

Katika maadhimisho hayo Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Jabir Shekimweri, Wanajeshi wa JKT toka Kikosi cha Mpwapwa, Kamati ya Ulinzi na  Usalama, Waheshimiwa Madiwani, Wafanyakazi wa Umma na wananchi wamejumuika kwa pamoja na kufanya shughuli zote za usafi katika maeneo yote yaliyopangwa. 

Kwa ujumla muitikio ulikuwa ni mzuri na hivyo usafi ulifanyika ipasavyo na kufanya maeneo yote kuwa safi.

Katika hotuba yake Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa amewataka wananchi na wadau wote kwa ujumla kujitokeza kwa wingi kama ilivyo katika siku hii ya leo katika siku ya usafi ya Jumamosi ya tarehe 28 Julai 2018 ili usafi uimalike. Pia ameongeza kuwa usafi uwe ni utamaduni wetu ambapo kila siku tufanye usafi katika maeneo yetu ya kazi pamoja na makazi.

Mhe. Jabir Shekimweri Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa (kulia) na Mhe. George Fuime Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa (kushoto) wakifanya usafi katika eneo la Hospitali ya  Mpwapwa  katika maadhimisho ya Siku ya Mashujaa tarehe 25 Julai 2018. (Picha. Na. Shaibu J. Masasi, Afisa TEHAMA - Mpwapwa)

Wafanyakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa pamoja na wananchi wakifanya usafi katika eneo la mnara wa mashujaa katika maadhimisho ya Siku ya Mashujaa tarehe 25 Julai 2018.

 (Picha. Na. Shaibu J. Masasi, Afisa TEHAMA - Mpwapwa)

Wanajeshi wa JKT kikosi cha Mpwapwa pamoja na wananchi wakifanya usafi katika eneo la kuzunguka Soko Kuu la Mpwapwa Mjini katika maadhimisho ya Siku ya Mashujaa tarehe 25 Julai 2018.

 (Picha. Na. Shaibu J. Masasi, Afisa TEHAMA - Mpwapwa)

Mhe. Jabir Shekimweri Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa akichangia damu kwa hiari katika Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa mara baada ya kumaliza zoezi la Usafi katika Siku ya Mashujaa tarehe 25 Julai 2018. 

                        (Picha. Na. Shaibu J. Masasi, Afisa TEHAMA - Mpwapwa)

Baadhi ya Wanajeshi wa JKT wakiwa katika foleni ya uchangiaji damu kwa hiari katika Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa mara baada ya kumaliza zoezi la Usafi katika Siku ya Mashujaa tarehe 25 Julai 2018. 

               (Picha. Na. Shaibu J. Masasi, Afisa TEHAMA - Mpwapwa)

Mkuu wa Jeshi la Polisi wilaya ya Mpwapwa Afande Mafuru (wa kwanza kulia) na wanajeshi wa JKT kikosi cha Mpwapwa wakifanya usafi katika eneo la kuzunguka Soko Kuu la Mpwapwa Mjini katika maadhimisho ya Siku ya Mashujaa tarehe 25 Julai 2018.  (Picha. Na. Shaibu J. Masasi, Afisa TEHAMA - Mpwapwa)

 Kamanda  Karuma wa jeshi la JKT Wilaya ya Mpwapwa akichangia damu kwa hiari katika Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa mara baada ya kumaliza zoezi la Usafi katika Siku ya Mashujaa tarehe 25 Julai 2018 (Picha. Na. Shaibu J. Masasi, Afisa TEHAMA - Mpwapwa)


Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye usahili MpwapwaDC June 27, 2022
  • Tangazo la nafasi za kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa. 2022 April 20, 2022
  • Tangazo la Nafasi za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa May 2022 May 31, 2022
  • Tangazo la kuahirishwa kwa Usahili Halmashauri ya Mpwapwa June 22, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • NORISH NA WAKULIMA WILAYA YA MPWAPWA

    May 06, 2025
  • VIONGOZI KUTOKA OFISI YA MAKAMU WA RAIS ZANZIBAR WATEMBELEA MIRADI YA MFUKO WA JIMBO MPWAPWA

    May 09, 2025
  • FUM YAFANYA ZIARA MIRADI YA KIMAENDELEO

    April 29, 2025
  • MAADHIMISHO YA MEI MOSI YAFANYIKA SINGIDA

    May 01, 2025
  • Tazama zote

Video

Video ya Mpango wa Uuzaji wa Viwanja Eneo la Mazae Block "E" katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa -2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa
  • Muundo wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani
  • Ratiba ya Vikao vya Madiwani

Viunganishi Linganishi

  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Wizara ya Fedha na Mipango
  • Utumishi portal
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu Teknolojia na Sayansi
  • Sekretarieti ya Ajira

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mpwapwa - Dodoma, Tanzania

    Anwani: S.L.P 12

    Simu: 255 26 2320122/2320

    Simu ya Kiganjani: 0684705551

    Barua pepe: info@mpwapwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovutii

Copyright © 2021 Mpwapwa District Council . All rights reserved.