• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mpwapwa District Council
Mpwapwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
        • Fedha
        • Biashara
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Mali asili
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Usafi na Mazingira
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Habari Mawasiliano na Tehama
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Nyuki
    • Mamlaka
      • Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mpwapwa
      • Mamlaka ya Maji Mpwapwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashuri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa mbali mbali
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo mbali mbali
    • Simulizi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video mbali mbali
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Mkuu wa Wilaya Asifu Kupanda kwa Mapato Mpwapwa

Posted on: November 7th, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Jabir Shekimweri leo katika kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa kilichofanyika katika Ukmbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa ameliambia Baraza hilo kuwa anaimani kubwa kwa sasa na utendaji  wa Mkuregenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa. Maneno hayo yamejili baada ya wenyevit wa kamati mbalimabli kuwasilisha taarifa zao ikiwepo kamati ya  Fedha Uongozi na Mipango (FUM) kuwasilisha taarifa ya hali ya Ukusanyaji wa mapato na kuongezeka kwa mapato.

Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa wakiwa kakiimba Wimbo wa Taifa kabla ya kuanza kikao cha Baraza la Madiwani

 Mhe. Kimweri ameeleza kuwa "Nia yangu ni kuiona Halmasahuri ya Wilaya ya Mpwapwa inasongambele katika ukusanyaji wa mapato na kuthibiti mianya ya upotevu wa mapato, hakika katika mapato nitasimamia kwa thati. Kwanza nimpe pongezi Mkurugenzi Mtendaji wa Halmasshauri ya Wilaya ya Mpwapwa na Menejimenti yake pamoja na waheshimiwa madiwani kwa kushirikiana kuweka mikakati mizuri ya ukusanyaji wa mapato, mapaka sasa ni robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2018/2019 Mpwapwa imefikia alisimia 33.4 na imevuka lengo la asilimia 25 kwa kila robo mwaka." Ameongeza kuwa hapa sasa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa inaenda vizuri katika ukusanyaji wa mapato na tutafikia malengo yetu.

 Pia Mkuu wa Wilaya ameonya kuwa atakuwa makali na kuchukua hatua kali za kisheria kwa mtumishi au mtu yeyote atakayehujumu jitihada za ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa

Vile vile ameeleza jitihada alizozifanya katika kuunga mkono katika suala ukusanyaji na uthibiti wa mapato ni pamoja na Kwenda Dar es Salaam kwa Mkurugenzi wa Kampuni ya Dayone Softcom Technologies kununua POS 30 aina ya TELPO TPS 390 kwa mali kauli (mkopo) na kuruhusu askari polisi kushirikiana na wataalam wa Halmashauri katika kuthibiti utoroshaji wa mapato wakati wa usiku.

Mheshimiwa Hakimu wa Mahakama ya Wilaya akimuapisha Mhe. Diwani wa Kata ya Wangi baada ya diwani wa kwanza kufariki.

Mkuu wa Wilaya ametoa taarifa Kliniki Tembezi iliyofanyika katika Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa kuanzia tarehe 21 Octoba  hadi 28 Octoba 2018 ambapo madaktari bingwa pamoja na wasaidizi wao toka Dodoma Hospitali ya Mkoa, Hospitali ya Benjamin Mkapa Dodoma na Muhimbili walifika na jumla yao ilikuwa zaidi ya 70 na walifanikiwa kutoa tiba kwa wagonjwa zaidi ya 2,000 wenye magonjwa mbalimbali. Mhe. Kimwei  ameomba Idara ya Afya iendelee kuratibu zoezi hili ili liweze kuendelea kwa kipindi kingine kwa sababu inaonyesha wananchi wanahitaji kwa wingi huduma hii.

Aidha amewatangazia fursa madaktari bingwa ya kilimo cha korosho katika Halmashauri ya wilaya ya Mpwapwa na amewahaidi kila daktari atapewa ekari moja bure, Madaktari bingwa hao wamekubali kuanza kilimo cha korosho Mpwapwa na kwa kuanzia kila daktari amehitaji ekari 10 kwa kununua japo kila mmoja atapewa ekari moja bure. Mpaka sasa madaktari bingwa wanaohitaji kulima kilimo cha zao la korosho Mpwapwa wamefikia 100 na wengine wanaendelea kutoa ahadi ya kuhita mashamba.

Waheshimiwa madiwani wakiwa katika kikao cha Baraza la Madiwani

Pia, Mkuu wa Wilaya ametoa wito kila kata na taasisi za serikali kuanzisha mashamba ya zao la korosho na kuweka sheria ndogo kwa wale watakaoharibu au kulishia mifugo katka mashamba ya korosho na kusababisha uharibifu wa mikorosho hatua zichukuliwe dhidi yao.

Kutokana na ushaushi huu wa Mkuu wa Wilaya,  Mwenyekiti wa Halmasahuri ya Mpwapwa Mhe. Donath S. Nghwenzi amempongeza Mkuu wa Wilaya kwa kuijali na kuwa na nia njema na Wilaya ya Mpwapwa na amehaidi kusimamia kikamilifu masuala yote muhimu na kuzingatia ushauri uliotolewa na Mkuu wa wilaya katika zao la korosho na ukusanyaji wa mapato.

Na: Shaibu J. Masasi, Afisa TEHAMA - Mpwapwa.


Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye usahili MpwapwaDC June 27, 2022
  • Tangazo la nafasi za kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa. 2022 April 20, 2022
  • Tangazo la Nafasi za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa May 2022 May 31, 2022
  • Tangazo la kuahirishwa kwa Usahili Halmashauri ya Mpwapwa June 22, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • NORISH NA WAKULIMA WILAYA YA MPWAPWA

    May 06, 2025
  • VIONGOZI KUTOKA OFISI YA MAKAMU WA RAIS ZANZIBAR WATEMBELEA MIRADI YA MFUKO WA JIMBO MPWAPWA

    May 09, 2025
  • FUM YAFANYA ZIARA MIRADI YA KIMAENDELEO

    April 29, 2025
  • MAADHIMISHO YA MEI MOSI YAFANYIKA SINGIDA

    May 01, 2025
  • Tazama zote

Video

Video ya Mpango wa Uuzaji wa Viwanja Eneo la Mazae Block "E" katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa -2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa
  • Muundo wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani
  • Ratiba ya Vikao vya Madiwani

Viunganishi Linganishi

  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Wizara ya Fedha na Mipango
  • Utumishi portal
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu Teknolojia na Sayansi
  • Sekretarieti ya Ajira

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mpwapwa - Dodoma, Tanzania

    Anwani: S.L.P 12

    Simu: 255 26 2320122/2320

    Simu ya Kiganjani: 0684705551

    Barua pepe: info@mpwapwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovutii

Copyright © 2021 Mpwapwa District Council . All rights reserved.