• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mpwapwa District Council
Mpwapwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
        • Fedha
        • Biashara
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Mali asili
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Usafi na Mazingira
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Habari Mawasiliano na Tehama
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Nyuki
    • Mamlaka
      • Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mpwapwa
      • Mamlaka ya Maji Mpwapwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashuri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa mbali mbali
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo mbali mbali
    • Simulizi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video mbali mbali
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Mkuu wa Wilaya Afungua Kikao cha Kampeni ya Chanjo ya Magonjwa Hatari

Posted on: October 11th, 2019

(Na: Shaibu J. Masasi, Afisa TEHAMA - Mpwapwa)

Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Jabir Shekimweri amefungua Kikao cha maandalizi ya Kampeni ya Chanjo ya Magonjwa hatari ya Surua, Rubella na Polio. Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Mkuu wa Wilaya na kuhudhuriwa na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa Mhe. George Fuime, baadhi ya waheshimiwa madiwani, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa Ndugu. Paul Sweya, Wajumbe wa kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, Wakuu wa idara na wataalam wa Afya akiwemo Mganga Mkuu wa Wilaya Daktari. Archard Rwezaula.

Akiwasilisha taarifa katika kikao hicho Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Daktari. Rwezaula amesema " Wilaya ya Mpwapwa ni miongoni mwa wilaya zinazoshiriki zoezi la uendeshaji wa kampeni ya chanjo ya kitaifa za Surua, Rubella na Polio ya sindano kwa watoto chini ya miaka mitano (5)" . Pia ameongeza kuwa "Watoto wanaolengwa katika zoezi hili ni wale walio na umri kati ya miezi 9 hadi miezi 59 hawa watapatiwa chanjo ya Surua na idadi yao wapata watoto 55,603 na watoto wanaostahili kupata chanjo ya Polio ya sindano ni wenye umri kati ya miezi 18 hadi 42 (yaani mwaka mmoja na nusu hadi miaka mitatu na nusu) ambao wapo 26,538".

Wajumbe waliohudhuria kikao cha Kampeni ya Chanjo ya Surua, Rubella na Polio ya sindano wakisikiliza hotuba ya Mkuu wa Wilaya

Chanjo hii itaanza tarehe 17/10/2019 hadi tarehe 21/10/2019 ambapo itachukua muda wa siku tano katika utekelezaji wake; na maeneo yatakayohusika na utoaji wa chanjo ni vituo vya kudumu ambavyo ni zahanati, Vituo vya afya, Hospitali na Vituo vya Kuhamahama hasa sehemu ambazo hakuna zahanati inaweza kutolewa kwenye ofisi za shule, kijiji, sokoni au Godown kadri ya mazingira yatavyoruhusu ili kuhakikisha kila mlengwa amefikiwa.

Akiwasilisha mada ya dalili na madhara ya magonjwa haya Ndugu Flugence Temu ambaye pia ni Mratibu wa Chanjo Wilaya ya Mpwapwa amesema kuwa: Magonjwa haya kwa ujumla yana madhara  makubwa kwa jamii na ametoa wito kwa jamii kujitokeza kwa wingi kupata chanjo hizi. Akitolea mfano wa dalili za Ugonjwa wa surua ni: homa, mafua na kikohozi kwa mtoto kwa siku chache za mwanzo, macho yanakuwa mekundu na hutoa majimaji, vipele vidogo vidogo hutokea ambavyo huanzia paji la uso, nyuma ya masikio na kusambaa usoni na mwili mzima. Pia madhara ya surua ni makubwa  kama vile: masikio kutoa usaha ambao huweza kusababisha kutosikia, vidonda vya macho vinavyoweza kusababisha upofu, nimonia, utapiamlo, kuvimba ubongo na kifo.

Aidha Ndug. Temu ameendelea kuzitaja dalili na madhara ya ugonjwa wa rubella; ambazo dalili zake ni:  vipele vidogo vidogo, homa, macho kuwa mekundu, uchvu wa mwili, vidonda kooni, uvimbe kwenye matezi na mafua. Madhara ya Rubella ni: matatizo ya moyo, kutosika vizuri, kupata mtoto wa jicho, maambukizi kwenye ubongo na mishipa ya fahamu.

Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Shekimweri amepongeza utangulizi wa Mganga Mkuu wa Wilaya kuwa amegusa nyanja zote muhimu katika shughuli nzima, pia amempongeza Ndugu. Temu kwa kuwasilisha mada vizuri na kuanisha madhara yatakayopatikana kama watoto wasipopata chanjo hizi.

Aidha Mkuu wa Wilaya ametoa wito kwa wananchi wote kujitokeza kwa wingi ili kuwapeleka watoto wao ili wapate chanjo hizi. Pia amesisitiza kuwa wajumbe waliopatiwa mafunzo au kujengewa uelewa wanatakiwa kuwa mabalozi wazuri wa kuelezea umuhimu wa chanjo hizi kwa jamii na sio kupotosha.

Kauli Mbiu ya kampeni hii ya Chanjo kwa mwaka huu 2019 ni "Chanjo ni kinga kwa pamoja tuwakinge"

Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye usahili MpwapwaDC June 27, 2022
  • Tangazo la nafasi za kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa. 2022 April 20, 2022
  • Tangazo la Nafasi za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa May 2022 May 31, 2022
  • Tangazo la kuahirishwa kwa Usahili Halmashauri ya Mpwapwa June 22, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • NORISH NA WAKULIMA WILAYA YA MPWAPWA

    May 06, 2025
  • VIONGOZI KUTOKA OFISI YA MAKAMU WA RAIS ZANZIBAR WATEMBELEA MIRADI YA MFUKO WA JIMBO MPWAPWA

    May 09, 2025
  • FUM YAFANYA ZIARA MIRADI YA KIMAENDELEO

    April 29, 2025
  • MAADHIMISHO YA MEI MOSI YAFANYIKA SINGIDA

    May 01, 2025
  • Tazama zote

Video

Video ya Mpango wa Uuzaji wa Viwanja Eneo la Mazae Block "E" katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa -2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa
  • Muundo wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani
  • Ratiba ya Vikao vya Madiwani

Viunganishi Linganishi

  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Wizara ya Fedha na Mipango
  • Utumishi portal
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu Teknolojia na Sayansi
  • Sekretarieti ya Ajira

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mpwapwa - Dodoma, Tanzania

    Anwani: S.L.P 12

    Simu: 255 26 2320122/2320

    Simu ya Kiganjani: 0684705551

    Barua pepe: info@mpwapwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovutii

Copyright © 2021 Mpwapwa District Council . All rights reserved.