• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mpwapwa District Council
Mpwapwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
        • Fedha
        • Biashara
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Mali asili
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Usafi na Mazingira
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Habari Mawasiliano na Tehama
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Nyuki
    • Mamlaka
      • Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mpwapwa
      • Mamlaka ya Maji Mpwapwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashuri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa mbali mbali
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo mbali mbali
    • Simulizi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video mbali mbali
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Bilinith Mahenge kufungua Mkutano wa Wadau wa Elimu Wilayani Mpwapwa

Posted on: January 17th, 2018

Mkutano wa Wadau wa Elimu wilayani Mpwapwa hufanyika kila mwaka na ulianza rasmi mwaka 2017, ila kwa mwaka huu 2018 pamoja na mambo mengine mkutano huu ulihusisha wadau mbalimbali kama vile viongozi wa serikali, wanasiasa, taasisi, dini, wafanyabiashara, walimu, wafanyakazi wa kada zote, wanafunzi na vijana toka Chuo Kikuu cha Dodoma ambao ni wazawa wa Mpwapwa. 

                      Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Ndg. Jabir Shekimweri akitambulisha meza kuu katika Mkutano wa Wadau wa Elimu kwenye Ukumbi wa Chuo cha Ualimu Mpwapwa.

Madhumuni ya Mkutano huu ni kutathmini matokeo ya mitihani (darasa la nne, la saba, kidato cha pili na kidato cha nne), kuibua changamoto zinazoikabili sekta ya  elimu na kuweka mikakati ya kuzitatua changamoto hizo kwa kupata mawazo mbalimbali toka kwa wadau wa elimu. Katika tathmini ya matokeo ya mitihani ya  mwaka 2017: shule, kata, walimu na wanafunzi waliofanya vizuri walipata zawadi mbalimbali kama vile pesa taslim, vitambaa vya suti, vyeti, vyombo vya nyumbani na luninga. Pia shule na kata zilizofanya vibaya walituzwa bendera nyeusi na vinyago kama ishara ya kufanya vibaya na wanahimizwa kujitahidi ili kupata matokeo mazuri. 

                  Wadau wa Elimu wakiwa katika Ukumbi wa Chuo cha Ualimu Mpwapwa tayari kwa Majadiliano

Katika mkuto wa mwaka huu Mgeni rasmi ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Bilinith Mahenge ambaye katika hotuba yake alipongeza kuanzishwa kwa mkutano wa wadau wa Elimu na ameziagiza Halmashauri zote za mkoa wa Dodoma kufanya mkutano kama huu kabla ya mwishoni mwa mwezi Januari mwaka 2018 kama huu ili kubaini changamoto za elimu na kuzitafutia uvumbuzi. Aidha amesema kuwa elimu ni ya msingi sana hivyo wazazi na wadau mbalimbali wawekeze kwenye elimu kwa kuwawezesha wanafunzi katika chakula na mahitaji muhimu kwa kuwa serikali inatoa Elimu bure. 

Pia ameupongeza uongozi wa Wilaya ya Mpwapwa kwa kufanya vizuri katika jitihada za kuinua taaluma, akitolea mfano katika matokeo ya mitihani ya kumaliza Elimu ya Msingi (darasa la saba) mwaka 2017 wilaya ya Mpwapwa ilishika nafasi ya 2, kwa kufaulisha 63.68% kimkoa  wakati mwaka 2016 ilipata  58.4% ilishika nafasi ya 7 kimkoa, aidha amelezela kwa upande wa Elimu sekondari katika matokeo ya kidato cha pili mwaka 2017 ufaulu ulikuwa 92%.

Vile vile amesema kuwa anazifahamu changamoto za madawati, madarasa, upungufu wa walimu, utoro na mimba, hivyo wadau wa elimu wa  wajadili namna ya kutatua changamoto hizo kwa kubuni mikakati mipya ya kutatua. Pia amependekeza walimu wanatakiwa kuhamishwa kwenda katika maeneo ambayo hayana walimu wa kutosha kwakuwa kuna baadhi ya shule na halmashauri zina walimu wa ziada wengi.

Sambamba na hilo ameutaka uongozi wa Halmashauri ya Mpwapwa kutembelea maeneo ya kutolea huduma kwa maana shule ili kubaini changamoto zinazozikabili shule na kuzitatua mara moja ili kuwatia moyo wa kufanyakazi kwa bidii.

        Wadau wa Elimu wakiwa katika Ukumbi wa Chuo cha Ualimu Mpwapwa wakisikiliza kwa umakini hotuba ya Mgeni rasmi Mkuu wa mkoa wa Dodoma.

Bofya hapa chini kupata hotuba mbalimbali.

Tathmini ya matokeo ya idara ya elimu msingi katika mkutano wa wadau wa elimu Januari 2018.ppt

Tathmini ya matokeo ya idara ya elimu sekondari katika mkutano wa wadau wa elimu Januari 2018.pptx

Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye usahili MpwapwaDC June 27, 2022
  • Tangazo la nafasi za kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa. 2022 April 20, 2022
  • Tangazo la Nafasi za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa May 2022 May 31, 2022
  • Tangazo la kuahirishwa kwa Usahili Halmashauri ya Mpwapwa June 22, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • NORISH NA WAKULIMA WILAYA YA MPWAPWA

    May 06, 2025
  • VIONGOZI KUTOKA OFISI YA MAKAMU WA RAIS ZANZIBAR WATEMBELEA MIRADI YA MFUKO WA JIMBO MPWAPWA

    May 09, 2025
  • FUM YAFANYA ZIARA MIRADI YA KIMAENDELEO

    April 29, 2025
  • MAADHIMISHO YA MEI MOSI YAFANYIKA SINGIDA

    May 01, 2025
  • Tazama zote

Video

Video ya Mpango wa Uuzaji wa Viwanja Eneo la Mazae Block "E" katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa -2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa
  • Muundo wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani
  • Ratiba ya Vikao vya Madiwani

Viunganishi Linganishi

  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Wizara ya Fedha na Mipango
  • Utumishi portal
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu Teknolojia na Sayansi
  • Sekretarieti ya Ajira

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mpwapwa - Dodoma, Tanzania

    Anwani: S.L.P 12

    Simu: 255 26 2320122/2320

    Simu ya Kiganjani: 0684705551

    Barua pepe: info@mpwapwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovutii

Copyright © 2021 Mpwapwa District Council . All rights reserved.