• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mpwapwa District Council
Mpwapwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
        • Fedha
        • Biashara
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Mali asili
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Usafi na Mazingira
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Habari Mawasiliano na Tehama
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Nyuki
    • Mamlaka
      • Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mpwapwa
      • Mamlaka ya Maji Mpwapwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashuri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa mbali mbali
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo mbali mbali
    • Simulizi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video mbali mbali
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

MAKAMO WA PILI WA RAIS ZANZIBAR AONGOZA IBADA YA KUMUOMBEA DUA HAYATI KARUME

Posted on: April 7th, 2025

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Alhaj Hemed Suleiman Abdulla amewaongoza viongozi wa serikali, chama, wanafamilia, waislamu na wananchi wa Zanzibar kwenye dua maalum (hitma) ya kumuombea aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Zanzibar, Marehemu Sheikh Abeid Amani Karume

Alhaj Hemed aliongoza hafla hiyo kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt Hussein Ali Mwinyi, hafla iliyofanyika Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui mjini Zanzibar.

Katika hafla hiyo, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alipata fursa ya kuzuru kaburi la hayati mzee Karume ambapo viongozi wa madhehebu mbalimbali walipata fursa ya kumuombea dua kiongozi huyo.

Akizungumza kwa niaba ya Mufti Mkuu wa Tanzania, Naibu Kadhi Mkuu wa Tanzania, Sheikh Khamis Juma amesema ni jambo jema na la faraja kuwakumbuka na kuwaombea dua viongozi waliotangulia mbele ya haki ambao walijitoa katika kulipigania Taifa.

Sheikh Khamis amewataka wananchi kuendeleza umoja, amani na mshikamano mambo ambavyo vilisimamiwa na viongozi waasisi wa Zanzibar na ndio chachu ya maendeleo yaliyofikiwa hapa nchini.

Akimzungumzia hayati Mzee Karume, Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Stephen Masato Wasira amesema kiongozi huyo alijitoa katika kuwapigania wazanzibari kuondokana na dhuluma pamoja na kusimamia haki, usawa na uzalendo katika kulijenga Taifa na ndio sababu kubwa ya kufanyika kwa mapinduzi Matukufuya mwaka 1964.

Wasira amesema suala la elimu na matibu bure lilipewa kipaombele na Mzee karume ikiwa ni falsafa yake ya kupingana na adui ujinga, maradhi na njaa jambo ambalo linaendelezwa na viongozi waliopo sasa madarakani.

Katibu mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar ndugu Khamis Abdalla Said amesema Marehemu Mzee Karume ameacha alama katika sekta ya elimu ambapo maendeleo makubwa ya elimu yaliyopo sasa yanatokana na misingi imara iliyoekwa na kiongozi huyo.

Alisema lengo la Mzee Karume kutangaza elimu bure lilikuwani  kuhakikisha watoto wa wakwezi na wakulima wanapata elimu bila ya malipo ili kujenga Taifa imara la baadae jambo linaloendelea kuenziwa na viongozi waliopo madarakani.


Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye usahili MpwapwaDC June 27, 2022
  • Tangazo la nafasi za kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa. 2022 April 20, 2022
  • Tangazo la Nafasi za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa May 2022 May 31, 2022
  • Tangazo la kuahirishwa kwa Usahili Halmashauri ya Mpwapwa June 22, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • NORISH NA WAKULIMA WILAYA YA MPWAPWA

    May 06, 2025
  • VIONGOZI KUTOKA OFISI YA MAKAMU WA RAIS ZANZIBAR WATEMBELEA MIRADI YA MFUKO WA JIMBO MPWAPWA

    May 09, 2025
  • FUM YAFANYA ZIARA MIRADI YA KIMAENDELEO

    April 29, 2025
  • MAADHIMISHO YA MEI MOSI YAFANYIKA SINGIDA

    May 01, 2025
  • Tazama zote

Video

Video ya Mpango wa Uuzaji wa Viwanja Eneo la Mazae Block "E" katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa -2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa
  • Muundo wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani
  • Ratiba ya Vikao vya Madiwani

Viunganishi Linganishi

  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Wizara ya Fedha na Mipango
  • Utumishi portal
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu Teknolojia na Sayansi
  • Sekretarieti ya Ajira

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mpwapwa - Dodoma, Tanzania

    Anwani: S.L.P 12

    Simu: 255 26 2320122/2320

    Simu ya Kiganjani: 0684705551

    Barua pepe: info@mpwapwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovutii

Copyright © 2021 Mpwapwa District Council . All rights reserved.