• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mpwapwa District Council
Mpwapwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
        • Fedha
        • Biashara
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Mali asili
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Usafi na Mazingira
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Habari Mawasiliano na Tehama
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Nyuki
    • Mamlaka
      • Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mpwapwa
      • Mamlaka ya Maji Mpwapwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashuri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa mbali mbali
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo mbali mbali
    • Simulizi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video mbali mbali
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Mpwapwa DC yatenga Siku Maalumu ya kazi za Maendeleo kwa Wananchi

Posted on: November 29th, 2017

 “Uhuru na Kazi “, “Uhuru na Maendeleo”, “Uhuru na Umoja”, “Kilimo cha Kufa na Kupona”...... Tanzania ya Viwanda

Tangu kupatikana kwa uhuru nchini mwaka 1961 serikali iliweka msisitizo mkubwa kwa jamii kujitegemea na kuhakikisha kila mwananchi anashiriki kikamilifu katika kazi za kujenga taifa. Ikumbukwe kuwa Kampeni mbalimbali zenye ujumbe maalum wa kuhimiza shughuli za kujitegemea na uelimishaji zilitumika mfano:  “Uhuru na Kazi “, “Uhuru na Maendeleo”, “Uhuru na Umoja”, “Kilimo cha Kufa na Kupona”. Katika kuleta ufanisi wa juhudi hizo viongozi wakuu wa serikali  na mashirika mbalimbali  walishiriki kwa vitendo katika kazi za maendeleo ya kijamii na kiuchumi wakiwa kama vielelezo vya kuhamasisha wananchi  kushiriki kikamilifu.

Siku za hivi karibuni imeonyesha kuwa jamii imesahau majukumu yao na kuachia serikali hali inayosababisha maendeleo ya wananchi kurudi nyuma. Serikali ya awamu ya tano imedhamiria kuamsha na kukuza ari ya wananchi kufanya kazi kwa bidii. Halmashauri ya wilaya Mpwapwa imepanga siku Maalum ya Kazi za Maendeleo ili kuinua ari ya wananchi kujitolea na kushiriki katika kazi za maendeleo katika kila kijiji iwe ni JUMATANO ya kila wiki. Siku hiyo itatumika na   wananchi katika vijiji vyao kupanga shughuli kwa pamoja na kujiletea maendeleo yao wenyewe.

Afisa maendeleo (W)  Khamlo Njovu  anatanabaisha kuwa uwepo wa siku maalumu ya kufanya kazi  una umuhimu Umuhimu wa kuanzishwa kwa siku Maalum ya kuinua ari ya jamii kumezingatia mahitaji mbalimbali ya kikatiba, Kisera, Sheria ya Nguvu Kazi ya mwaka 1983, hali halisi ya ongezeko la mahitaji ya jamii, kasi ya ukuaji wa uchumi na Mipango mbalimbali ya maendeleo ya Taifa. Utekelezaji wa siku hii unatarajiwa kuleta tija katika mambo yafuatayo:

A : KIJAMII

  • Kutoa fursa ya kuleta hamasa kwa wananchi kuwa na tabia ya kushiriki kwa hiari yao na kufanya kazi kwa bidii.
  • Kuwezesha jamii kuona umuhimu wa kushirikisha makundi yote katika shughuli za maendeleo na kuachana na mila, desturi na mitazamo zinazobagua  baadhi ya makundi katika jamii kushiriki katika kazi za maendeleo
  • Kuwezesha jamii kujiamini na kushikamana katika kutafuta ufumbuzi wa changamoto zinazowakabili na kushiriki katika kuimarisha hali za maisha ya makundi maalum ya wanawake, wazee, watoto na watu wenye ulemavu
  • Kuwezesha ushiriki wa pamoja wa viongozi, wataalam na wananchi katika kazi za maendeleo kulingana na ratiba za maeneo husika.
  • Kuamsha ari ya jamii kumiliki shughuli za  miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao (sense of ownership)

B : KIUCHUMI

  • Kuwezesha jamii kujitathimini kuhusu maendeleo ya sehemu zao husika na kuibua miradi itakayopunguza kero za muda mrefu zinazowakabili
  • Kuinua ari na moyo wa wananchi na viongozi wa ngazi mablimbali kujitolea kufanya kazi za maendeleo na kuchangia fedha na vifaa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya kujitegemea
  • Kuwezesha kukamilika kwa miradi ambayo kwa muda mrefu imeachwa bila kukamilika ikiwa ni pamoja na kuhakikisha uendelevu wa miradi hiyo Mfano, miradi ya ujenzi na Ukarabati wa miundo mbinu mbalimbali
  • Kuwezesha kuunda vikundi mbalimbali vya kijamii vya kiuchumi, mfano vikundi vya ujasiliamali, SACCO’s na VICOBA


Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye usahili MpwapwaDC June 27, 2022
  • Tangazo la nafasi za kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa. 2022 April 20, 2022
  • Tangazo la Nafasi za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa May 2022 May 31, 2022
  • Tangazo la kuahirishwa kwa Usahili Halmashauri ya Mpwapwa June 22, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • NORISH NA WAKULIMA WILAYA YA MPWAPWA

    May 06, 2025
  • VIONGOZI KUTOKA OFISI YA MAKAMU WA RAIS ZANZIBAR WATEMBELEA MIRADI YA MFUKO WA JIMBO MPWAPWA

    May 09, 2025
  • FUM YAFANYA ZIARA MIRADI YA KIMAENDELEO

    April 29, 2025
  • MAADHIMISHO YA MEI MOSI YAFANYIKA SINGIDA

    May 01, 2025
  • Tazama zote

Video

Video ya Mpango wa Uuzaji wa Viwanja Eneo la Mazae Block "E" katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa -2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa
  • Muundo wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani
  • Ratiba ya Vikao vya Madiwani

Viunganishi Linganishi

  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Wizara ya Fedha na Mipango
  • Utumishi portal
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu Teknolojia na Sayansi
  • Sekretarieti ya Ajira

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mpwapwa - Dodoma, Tanzania

    Anwani: S.L.P 12

    Simu: 255 26 2320122/2320

    Simu ya Kiganjani: 0684705551

    Barua pepe: info@mpwapwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovutii

Copyright © 2021 Mpwapwa District Council . All rights reserved.