• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mpwapwa District Council
Mpwapwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
        • Fedha
        • Biashara
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Mali asili
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Usafi na Mazingira
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Habari Mawasiliano na Tehama
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Nyuki
    • Mamlaka
      • Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mpwapwa
      • Mamlaka ya Maji Mpwapwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashuri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa mbali mbali
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo mbali mbali
    • Simulizi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video mbali mbali
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Katibu Tawala Aibana Kampuni ya Halotel Kulipa Malipo ya Minara

Posted on: March 27th, 2020

Na: Shaibu J. Masasi; Afisa TEHAMA - Mpwapwa Dc.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Sarah J. Komba amemuita Mkurugenzi wa Kampuni ya Simu za Mkononi ya Viettel Tanzania/Halotel tawi la Dodoma Ndugu. Tran The Hoang katika kikao kilichofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa. Kikao hicho kimehudhuriwa na Wananchi wa Kijiji cha Berege ambapo Mnara Umejengwa katika kijiji hicho na Kampuni ya Halotel ila hailipi mapato ya kijiji, Watu binafsi akiwemo Mzee  Mzee Sepetu ambaye Mnara wa Halotel umejengwa kwenye eneo lake lakini halipwi fedha, watendaji wa vijiji na kata za Berege na Matomondo.

Aidha kikao hicho kimedhuriwa na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa Ndugu. Paul M. Sweya pamoja na Wataalam toka Halmashauri ya Wiaya ya Mpwapwa akiwemo Afisa Ardhi, Mwanasheria na Afisa TEHAMA.

Katibu Tawala amefikia uamuzi huo kwa kuwa kampuni ya Halotel imekuwa ikilalamikiwa na watu binafsi na taasisi kuhusu mikataba yao ina vipengele vinavyombana mwananchi, kiasi cha fedha kinacholipwa kwa malipo ya kupangisha eneo lilijengwa mnara ni kidogo, wanapobomoa au kujenga mnara huwa hawafuati utaratibu wa kupata kibali, kutolipa malipo ya minara kwa wakati, pia migogoro ya ardhi iliyosababishwa na kujenga minara katika maeneo yasiyo sahihi au kuingia mkataba na kumlipa fedha mtu asiyekuwa mmiliki wa eneo.

Baada ya Majadiliano, Wawakilishi wa Kampuni ya Halotel akiwemo Mkurugeni wa Halotel tawi la Dodoma wameshindwa kutoa majibu ya kuridhisha  na kujitosheleza kwa wajumbe waliohudhiria kikao hicho kwa hoja zilizowasilishwa.

Wawakilishi wa taasisi na watu binafsi wenye madai mbalimbali kwa kampuni ya Halotel wakiwa na wawakilishi wa Kampuni ya Halotel katika kikao cha pamoja kilichoitishwa na Mhe. Sarah Komba (wa pili kushoto waliokaa meza kuu) Katibu Tawala Wilaya ya Mpwapwa

Baada ya Wawakilishi wa Kampuni ya Halotel kushindwa kujibu hoja zilizowasilishwa, Katibu Tawala ameiagiza kampuni ya Halotel  baada ya Mwezi Mmoja  katika kikao kijacho cha tarehe 20 Aprili 2020 walete majibu:- majibu yajikite katika Vipengele vya mikataba vikarekebishwe, mikataba katika minara yote ionekane na ijulikane kwa wamiliki halisi, kuongeza viwango vya  kodi/malipo kadri ilivyopendekezwa, kulipa kwa wakati malipo ya pango la minara, na kuleta nyaraka za ushahidi kuwa Mzee Sepetu alikuwa analipwa fedha za mnara kwa miezi ya nyuma. Pia ameongeza kuwa "katika kikao kijacho cha tarehe 20 Aprili 2020 nahitaji kumuona Mkurugenzi Mkuu wa Halotel anayeshughulikia mikataba yote ya minara Tanzania na awe na majibu ya hoja zote zilizotolewa ".

Hata hivyo Mhe. Sarah Komba ameipongeza Kampuni ya Halotel kwa kujenga minara 20 na kufanikisha mawasiliano ya mtandao huo maeneo yote ya Wilaya ya Mpwapwa. Pia ameongeza kuwa asilimia 90 ya wanatumia simu za mkono katika Wilaya ya Mpwapwa wanatumia laini za Halotel, hivyo kampuni hii inafanya vizuri katika sekta ya mawasiliano kwenye Wilaya yetu.

***Mwisho***

Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye usahili MpwapwaDC June 27, 2022
  • Tangazo la nafasi za kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa. 2022 April 20, 2022
  • Tangazo la Nafasi za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa May 2022 May 31, 2022
  • Tangazo la kuahirishwa kwa Usahili Halmashauri ya Mpwapwa June 22, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • NORISH NA WAKULIMA WILAYA YA MPWAPWA

    May 06, 2025
  • VIONGOZI KUTOKA OFISI YA MAKAMU WA RAIS ZANZIBAR WATEMBELEA MIRADI YA MFUKO WA JIMBO MPWAPWA

    May 09, 2025
  • FUM YAFANYA ZIARA MIRADI YA KIMAENDELEO

    April 29, 2025
  • MAADHIMISHO YA MEI MOSI YAFANYIKA SINGIDA

    May 01, 2025
  • Tazama zote

Video

Video ya Mpango wa Uuzaji wa Viwanja Eneo la Mazae Block "E" katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa -2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa
  • Muundo wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani
  • Ratiba ya Vikao vya Madiwani

Viunganishi Linganishi

  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Wizara ya Fedha na Mipango
  • Utumishi portal
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu Teknolojia na Sayansi
  • Sekretarieti ya Ajira

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mpwapwa - Dodoma, Tanzania

    Anwani: S.L.P 12

    Simu: 255 26 2320122/2320

    Simu ya Kiganjani: 0684705551

    Barua pepe: info@mpwapwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovutii

Copyright © 2021 Mpwapwa District Council . All rights reserved.