• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mpwapwa District Council
Mpwapwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
        • Fedha
        • Biashara
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Mali asili
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Usafi na Mazingira
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Habari Mawasiliano na Tehama
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Nyuki
    • Mamlaka
      • Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mpwapwa
      • Mamlaka ya Maji Mpwapwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashuri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa mbali mbali
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo mbali mbali
    • Simulizi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video mbali mbali
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa Yazindua Chanjo ya Saratani ya Mlango wa Kizazi

Posted on: May 30th, 2018

Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa yazindua mpango wa taifa wa utoaji wa chajo ya saratani ya shingo ya kizazi kwa wasichana wanye umri wa miaka 14 kama maelekezo ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto yanavyo hitaji. Chanjo hiyo imezinduliwa leo na kaimu Katibu Tawala wa Wilaya ya Mpwapwa Ndg. Apolonia Temu katika viwanja vya Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa leo tarehe 30/05/2018. Katika uzinduzi huo wananchi wote wamehudhuria pamoja na wanafunzi wa shule za msingi na sekondari za Mpwapwa Mjini. 

Wilaya ya Mpwapwa ni miongoni mwa wilaya ambayo inatekeleza zoezi la kitaifa la uzinduzi wa chanjo ya kuzuia Saratani ya Mlango wa kizazi kwa mabinti wenye umri wa miaka 14, Uzinduzi huu umefanyika  katika Hospitali ya wilaya  ambapo walengwa ni wanafunzi wa shule za msingi na sekondari za hapa mjini kama zifuatavyo: sekondari ya mwanakianga, Mazae, Mount Igovu, Ihala, Qeen Ester na Vighawe. Pamoja na uzinduzi huu zoezi hili linaendelea katika vituo vyote vya kutolea huduma vya Afya vikiwemo vya Serikali, Mashirika ya Dini na Binafsi.

Wanafunzi wakisubiri taratibu za kupimwa na kupewa chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi (Picha. Alutha Kimbe, Afisa TEHAMA - Mpwapwa)

katika hotuba yake Mgeni rasmi ambaye ni katibu tawala wa wilaya ya Mpwapwa amesema "Saratani ya mlango wa kizazi inachangiwa na vitu vingi ikiwemo kuanza kujamiana katika umri mdogo, kuwa na wapenzi wengi, kuwa na ndoa za mitala, kuzaa watoto wengi, na uvutaji wa sigara". Pia ameongeza kuwa dalili za saratani ya mlango wa kizazi mara nyingi hujitokeza ikiwa imeshasambaa mwilini. Zifuatazo ni baadhi ya dalili za saratani mfano; kutokwa damu ya hedhi bila mpangilio, kutokwa damu baada ya kujamiiana, maumivu ya mgongo, miguu na/au kiuno, kuchoka, kupungua uzito, kupungukiwa au kokosa hamu ya kula, kutokwa uchafu wa rangi ya kahawia au wenye damu kwenye uke, maumivu ya miguu au kuvimba.

Wasichana wenye umri wa miaka 14 ambao ni wanafunzi akipatiwa chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi wilayani Mpwapwa

Pia mgeni rasmi ameongeza kuwa dalili mbaya zaidi zinazoweza kujitokeza ni pamoja na kuishiwa damu, figo kushindwa kufanya kazi, kupatwa na fistula, na uvimbe wa tezi. Lengo hasa la kuanzisha chanjo hii ni kukinga mabinti wetu kutokana na madhara makubwa yanayoweza kuwapata ambayo husababisha vifo vingi kwa wanawake, na hivyo kuboresha afya za jamii ya wanawake Watanzania kwa ujumla. Uanzishwaji wa chanjo hii utahusisha pia Mkoa wetu.Walengwa wa chanjo hii kwa mwaka huu wa 2018 ni wasichana wote wanaotimiza miaka 14, ambao kwa wilaya yetu ya Mpwapwa tunatarajia kuchanja mabinti wapatao 4046.Katika uzinduzi huu tutaanza na shule zote za Sekondari zilizopo hapa mjini ambapo uzinduzi wake unafanyikia katika Hospitali ya wilaya. Kutokana na ratiba za shaule zoezi hili linatarajiwa kukamilika kablaya kufungwa kwa shule.Chanjo hii hutolewa kwa dose mbili yaani (dose 1wakati wowote dose ya pili baada ya miezi 6) Ndugu Wananchi/Wanafunzi. 

Wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wilayani Mpwapwa wakiwa katika uzinduzi wa chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi

Mwisho mgeni rasmi ametoa wito wa wananchi wote kwa ujumla kuwa na muamko wa kuwahamasisha wa watoto wao wakike wenye umri wa miaka 14 kupata kinga na waliozidi umri huu kuweza kupima saratani ya mlango wa kizazi. Ili kujilinda na saratani ya mlango wa kizazi, njia ya kwanza ni kupata chanjo ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi, kutokufanya ngono katika umri mdogo, kuepuka kubeba mimba katika umri mdogo. 

Napenda pia niwataarifu mkakati utakaotumika katika utoaji wa chanjo hii. Kutokana na uzoefu uliopatikana wakati wa majaribio ya utoaji wa chanjo hii Mkoani Kilimanjaro, chanjo hii itatolewa katika utaratibu wa kawaida katika vituo vyetu vya kutolea huduma za chanjo, baadhi ya shule zitakazochaguliwa, na baadhi ya maeneo katika jamii ambapo zitatolewa kwa njia za huduma za mkoba.Huduma hizi zitatolewa bila malipo katika vituo vya kutolea huduma za afya vya serikali na binafi.Chanjo hii imethibitishwa kuwa ni salama na haina madhara yoyote. Wizara yetu kwa kushirikiana na wadau tumejipanga vizuri kuhakikisha watoto wetu wanaondokana na tatizo hili.

Mganga mfawidhi wa hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa Daktari Hamza aliyesimama akiafafanua naman ya utoaji wa chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi katika uzinduzi wa chanjo hiyo 

Kwa taarifa zaidi pakua nyaraka hii hapa chini:

HOTUBA UZINDUZI WA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI.pdf

Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye usahili MpwapwaDC June 27, 2022
  • Tangazo la nafasi za kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa. 2022 April 20, 2022
  • Tangazo la Nafasi za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa May 2022 May 31, 2022
  • Tangazo la kuahirishwa kwa Usahili Halmashauri ya Mpwapwa June 22, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • NORISH NA WAKULIMA WILAYA YA MPWAPWA

    May 06, 2025
  • VIONGOZI KUTOKA OFISI YA MAKAMU WA RAIS ZANZIBAR WATEMBELEA MIRADI YA MFUKO WA JIMBO MPWAPWA

    May 09, 2025
  • FUM YAFANYA ZIARA MIRADI YA KIMAENDELEO

    April 29, 2025
  • MAADHIMISHO YA MEI MOSI YAFANYIKA SINGIDA

    May 01, 2025
  • Tazama zote

Video

Video ya Mpango wa Uuzaji wa Viwanja Eneo la Mazae Block "E" katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa -2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa
  • Muundo wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani
  • Ratiba ya Vikao vya Madiwani

Viunganishi Linganishi

  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Wizara ya Fedha na Mipango
  • Utumishi portal
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu Teknolojia na Sayansi
  • Sekretarieti ya Ajira

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mpwapwa - Dodoma, Tanzania

    Anwani: S.L.P 12

    Simu: 255 26 2320122/2320

    Simu ya Kiganjani: 0684705551

    Barua pepe: info@mpwapwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovutii

Copyright © 2021 Mpwapwa District Council . All rights reserved.