• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mpwapwa District Council
Mpwapwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
        • Fedha
        • Biashara
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Mali asili
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Usafi na Mazingira
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Habari Mawasiliano na Tehama
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Nyuki
    • Mamlaka
      • Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mpwapwa
      • Mamlaka ya Maji Mpwapwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashuri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa mbali mbali
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo mbali mbali
    • Simulizi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video mbali mbali
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Fundi Umeme Apewa Siku 5 Kukamilisha Kazi katika Kituo cha Afya

Posted on: December 31st, 2018

(Na: Shaibu J. Masasi, Afisa TEHAMA - Mpwapwa)

Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Jabir Shekimweri amefanya ziara katika kituo cha Afya cha Kibakwe kuona umaliziaji wa majengo ya kituo hicho unavyoendelea. Katika ukaguzi wa majengo yote mkuu wa wilaya ameona ujenzi unavyoendelea na hatua iliyofikia ni ya ukamilishaji tu na mafundi wako kazini. Katika nyumba ya Mganga ujenzi unaendelea na upo katika hatua ya kuwekwa milango.Pia katika nyumba hiyo Mkuu wa Wilaya amepewa maelezo na kamati ya ujenzi kuwa jengo halijafunywa nyaya za umeme (wiring).

Kutokana hali hii ya kutofungwa kwa nyaya za umeme katika nyumba hiyo ya mganga, Mkuu wa Wilaya amelazimika kumtafuta fundi umeme aliyepewa kazi hiyo kutaka kujua kwa nini hajakamilisha kazi. Fundi umeme alipoulizwa kwa nini hajakamilisha kazi, alieleza kuwa alikuwa analipwa kidogo kidogo na mpaka sasa amelipwa Shilingi Milioni ishirini na tano tu pamoja na ufundi. Wakati Mkataba unaonenyesha ni Shilingi Milioni ishirini na tisa tu pamoja na feni na Air condition (A.C). Kwa hiyo feni na AC ameshindwa kufunga kwa kuwa hakupewa fedha kwa ajili ya vifaa hivyo lakini pesa ya vifaa vya umeme na ufundi yote alilipwa.

Nyumba ya Mganga ambayo bado haijafungwa umeme katika Kituo cha Afya cha Kibakwe

Baada ya maelezo hayo ya fundi umeme, Mkuu wa Wilaya amemuagiza Fundi Umeme amalize kazi ya kufunga nyaya za umeme nyumba yote ya mganga kabla ya tarehe 5 Januari, 2019 na atakuja kukagua. Pia Mhe. Shekimweri amemueleza Fundi Umeme huyo kuwa "Serikali imeleta miradi hii kwa Local Fundis ili nao wapate fedha na kuthamini kazi zao nzuri wanazozifanya. Lakini kwa kutokuwa waaminifu kwa baadhi ya mafundi mtasababisha mkose kazi hizi za Serikali". amesema Mhe. Shekimweri.

Kwa upande mwingine, Mkuu wa Wilaya amekagua Jengo la Wagonjwa wa Nje (OPD) na kugundua kasoro kadha ikiwemo jengo kutokamilika katika hatua za umaliziaji katika milango ambapo mafundi walikuwa wakifunga milango. Pia kuna baadhi ya vigae vya sakafuni (tiles) vimewekwa vibaya, kuna baadhi ya kuta hazijamaliziwa kupigwa plasta wakati jengo lote limepakwa rangi.

Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Jabir Shekimweri (kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji Wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa Ndug. Paul Mamba Sweya (kulia) wakikagua majengo ya  Kituo cha Afya cha Kibakwe

Kufuatia hali hii ya jengo hilo la OPD kutokamilika na kuwa na kasoro nyingi, Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Shekimweri amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa Ndug. Paul Mamba Sweya kuhakikisha kasoro zote zinarekebishwa na jengo linakamilika kabla ya tarehe 15 Januari 2019, kwa kuwa tarehe hiyo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dtk. John Pombe Magufuli anatarajia kuzindua vituo vyote vya afya nzima na viaze kufanyakazi mara moja.

"Mimi kama Mkuu wa Wilaya ninayemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dtk. John Pombe Magufuli sitokubali kuona vituo vya afya vimezinduliwa Nchi nzima kwa ajili ya kutoa huduma alafu kituo cha Afya cha Kibakwe bado kipo katika ujenzi". amesisitiza Mhe. Shekimweri.

Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Jabir Shekimweri akikagua nafasi kubwa iliyoachwa wazi katii ya ukuta na tiles jengo la OPD katika Kituo cha Afya cha KIbakwe



Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye usahili MpwapwaDC June 27, 2022
  • Tangazo la nafasi za kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa. 2022 April 20, 2022
  • Tangazo la Nafasi za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa May 2022 May 31, 2022
  • Tangazo la kuahirishwa kwa Usahili Halmashauri ya Mpwapwa June 22, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • NORISH NA WAKULIMA WILAYA YA MPWAPWA

    May 06, 2025
  • VIONGOZI KUTOKA OFISI YA MAKAMU WA RAIS ZANZIBAR WATEMBELEA MIRADI YA MFUKO WA JIMBO MPWAPWA

    May 09, 2025
  • FUM YAFANYA ZIARA MIRADI YA KIMAENDELEO

    April 29, 2025
  • MAADHIMISHO YA MEI MOSI YAFANYIKA SINGIDA

    May 01, 2025
  • Tazama zote

Video

Video ya Mpango wa Uuzaji wa Viwanja Eneo la Mazae Block "E" katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa -2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa
  • Muundo wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani
  • Ratiba ya Vikao vya Madiwani

Viunganishi Linganishi

  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Wizara ya Fedha na Mipango
  • Utumishi portal
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu Teknolojia na Sayansi
  • Sekretarieti ya Ajira

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mpwapwa - Dodoma, Tanzania

    Anwani: S.L.P 12

    Simu: 255 26 2320122/2320

    Simu ya Kiganjani: 0684705551

    Barua pepe: info@mpwapwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovutii

Copyright © 2021 Mpwapwa District Council . All rights reserved.