• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mpwapwa District Council
Mpwapwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
        • Fedha
        • Biashara
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Mali asili
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Usafi na Mazingira
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Habari Mawasiliano na Tehama
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Nyuki
    • Mamlaka
      • Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mpwapwa
      • Mamlaka ya Maji Mpwapwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashuri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa mbali mbali
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo mbali mbali
    • Simulizi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video mbali mbali
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

BOT Yatoa Mafunzo ya Utambuzi wa Fedha Halali Mpwapwa

Posted on: February 28th, 2019

(Na: Shaibu J. Masasi, Afisa TEHAMA - Mpwapwa)
Benki Kuu ya Tanzania (BOT) leo imetoa mafunzo kwa watumishi, wanachuo, wanafunzi wa shule za sekondari na wananchi wa Wilaya ya Mpwapwa juu ya njia za kutambua fedha halali. Katika mafunzo haya yanamadhumuni ya kuwaabalisha wananchi katika kutambua fedha halali ili wasiweze kutapeliwa kirahisi kwa kupewa fedha bandia. Pia imeelezwa kuwa fedha bandia husababisa kudumaza uchumi wa mwanachi mmoja mmoja pamoja na Taifa kwa ujumla, zinasababisha watu kutofaka kazi au biashara kwa kuogopa kulipwa fedha bandia.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Mpwapwa Ndug. Sarah Komba (aliyesimama) akifungua mafunzo yanayoendeshwa na BOT ya kutambua fedha halali katika Ukumbi wa CCM Wilaya

Akifungua mafunzo haya Katibu Tawala wa Wilaya ya Mpwapwa Ndug. Sarah John Komba kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Jabir Shekimweri, amewataka wadau wote waliohudhuria kuwa wasikivu na makini katika kufuatilia mafunzo haya kwa kuwa yana umuhimu mkubwa katika jamii zetu. Pia Bi. Komba amesema "naomba muwe makini kwa kuwa
wananchi wengi hawana uelewa wa utambuzi wa  noti halali, hivyo ninyi mtakuwa walimu kwa wengine
".  Mwisho amewakaribisha wawezeshaji toka BOT kuanza kutoa mafunzo.

Mwezeshaji toka BOT akitoa mafunzo ya utambuzi wa fedha halali katika Ukumbi wa CCM Wilaya ya Mpwapwa

Mwezeshaji toka BOT baada ya kukaribisha, ametoa mafunzo ya kutambua noti halali:-Kuna njia tatu za kutambua noti halali za aina zote za Tanzania (1) Kwa kuangalia noti kwa macho (2) Kwa kupapasa (3) Kwa kutumia vifaa maalum
(1) Kwa kuangalia kwa macho.
 - Kuangalia picha mficho ya mwalimu Julius K. Nyerere.
 - Katika picha mficho ya mwalimu Julius K. Nyerere katika kidevu kumeandikwa thamani ya noti husika.
 - Kuangalia utepe wa mstali unaong'aa kama kioo.
 - Juu ya kichwa cha picha mficho ya Mwalimu Nyerere kuna nukta nukta ambazo ukiangalia kwa makini zitaunganika na kufanya tarakimu ya thamani ya fedha.
 - Nyuma ya fedha kuna picha ya twiga na inamng'ao kama dhahabu na huwa inabadilika kuwa kijani au bluu.
 
 (2) Kwa kupapasa
 - kupapasa pembeni ya noti, huwa kunakuwa kama kuna nundu nundu.
 - Chini ya maneno Benki Kuu ya Tanzania kuna maneno madogo yameandikwa fedha halali kwa malipo ya shilingi...... huwa yanakuwa yana nundu nundu.
 - chini ya picha mficho ya mwalimu nyerere kuna mistari ya V ukipapasa inakuwa na nundu nundu.
 -
(3) Kwa kutumia vifaa maalum (tochi ya mwanga wa bluu)
- Mulika tochi/taa ya mwanga wa bluu katika namba ya fedha, itaakisi mwanga kama reflectors.
- Mulika upande wa picha mficho ya mwalimu Julius K. Nyerere na utaona kiboksi kimeandikwa TZS na thamani ya noti husika.
-Mulika sehemu ya nyuma chini ya twiga utaona maua yanawaka.

Baada ya kufundishwa njia hizo tatu, washiriki waliruhusiwa kufanya utambuzi wa fedha halali kwa vitendo na kubaini fedha walizonazo zilikuwa halali.

Mshiriki Ndug. Baraka Msuya (aliyesimama) akielezea namna ya kutambua fedha halali wakati wa mafunzo ya BOT katika Ukumbi wa CCM Wilaya ya Mpwapwa

Mwezeshaji ametoa wito kuwa fedha zitunzwe benki na kama kina kiasi kidogo kwa ajili ya matumizi kutunzwe kwenye waleti na sio kuikunja katika pindo za nguo. Mwezeshaji aliomba mshiriki mmoja aelezee jinsi ya kutambua fedha halali ambapo Ndug. Baraka Msuya toka Ofisi ya Maendeleo ya Jamii alielezea kwa usahihi njia zote tatu za kutambua fedha halali na mafunzo yalifungwa.


Kwa maelezo zaidi soma vipeperushi vya BOT hapa chini


Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye usahili MpwapwaDC June 27, 2022
  • Tangazo la nafasi za kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa. 2022 April 20, 2022
  • Tangazo la Nafasi za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa May 2022 May 31, 2022
  • Tangazo la kuahirishwa kwa Usahili Halmashauri ya Mpwapwa June 22, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • NORISH NA WAKULIMA WILAYA YA MPWAPWA

    May 06, 2025
  • VIONGOZI KUTOKA OFISI YA MAKAMU WA RAIS ZANZIBAR WATEMBELEA MIRADI YA MFUKO WA JIMBO MPWAPWA

    May 09, 2025
  • FUM YAFANYA ZIARA MIRADI YA KIMAENDELEO

    April 29, 2025
  • MAADHIMISHO YA MEI MOSI YAFANYIKA SINGIDA

    May 01, 2025
  • Tazama zote

Video

Video ya Mpango wa Uuzaji wa Viwanja Eneo la Mazae Block "E" katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa -2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa
  • Muundo wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani
  • Ratiba ya Vikao vya Madiwani

Viunganishi Linganishi

  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Wizara ya Fedha na Mipango
  • Utumishi portal
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu Teknolojia na Sayansi
  • Sekretarieti ya Ajira

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mpwapwa - Dodoma, Tanzania

    Anwani: S.L.P 12

    Simu: 255 26 2320122/2320

    Simu ya Kiganjani: 0684705551

    Barua pepe: info@mpwapwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovutii

Copyright © 2021 Mpwapwa District Council . All rights reserved.