• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mpwapwa District Council
Mpwapwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
        • Fedha
        • Biashara
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Mali asili
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Usafi na Mazingira
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Habari Mawasiliano na Tehama
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Nyuki
    • Mamlaka
      • Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mpwapwa
      • Mamlaka ya Maji Mpwapwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashuri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa mbali mbali
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo mbali mbali
    • Simulizi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video mbali mbali
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Benki ya NMB Yatoa Msaada Siku ya Usafi Duniani

Posted on: September 15th, 2018

Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa leo imeadhimisha Siku ya Usafi Duniani kiwilaya ambapo kwa mara ya kwanza Nchi ya Tanzania imeadhimisha sikuku hiyo ambayo Dunia huadhimisha kila mwaka Septemba 15. Katika Sikukuu hiyo iliyoadhimishwa katika viwanja vya Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa zimeambatana na kufanya usafi katika mazingira ya Hospitali hiyo. Ndugu Gloria Balegu, Afisa Tarafa ya Mpwapwa Mjini ndio mgeni rasmi katika Sikukuu hiyo ya Usafi Duniani, akimuwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Jabir Shekimweri.

Mgeni rasmi Ndugu Gloria Balegu (wa kwanza kulia aliyesimama) ambae pia ni Afisa Tarafa wa Tarafa ya Mpwapwa Mjini akimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa akitoa hotuba katika Viwanja vya Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa.

Katika sikukuu hiyo Benki ya NMB tawi la Mpwapwa imetoa msaada wa vifaa vya kufanyia usafi kwa Uongozi wa Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa, akikabidhi msaada huo Ndugu Beatrice ambaye ni Meneja wa Benki ya NMB tawi la Mpwapwa amesema "Benki ya NMB tawi la Mpwapwa imeona ni vema iungane na Uongozi wa wilaya ya Mpwapwa katika kuadhimisha siku hii ya Usafi Duniani kwa kufanya usafi katika mazingira ya Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa na kutoa msaada wa vifaa vya usafi katika Hospitali hiyo". Aidha meneja huyo ameongeza kuwa Benki ya NMB imekuwa ikitoa misaada mingi ya kijamii kama kusaidia majanga, ujenzi na kuchangia huduma ya afya. Kwa leo Benki ya NMB tawi la Mpwapwa imetoa msaada wa vifaa vya usafi kama vile majembe, reki, mifagio, kwanja na tolori.

Pia meneja wa Benki ya NMB huyo amepata fursa ya kuwatangazia na kuwaelezea wananchi kwa kina kuhusu huduma mpya zinazotolewa na benki hiyo, huduma hiyo ni kama Kukopa pesa NMB ndani ya mwezi mmoja kabla ya mshahara kutoka (Salary Advance) na Akiba kwa wanafunzi.

Mgeni rasmi Ndugu. Gloria Balegu (wapili kulia) akikabidhiwa msaada wa vifaa vya usafi toka kwa meneja wa benki ya NMB tawi la Mpwapwa Ndugu. Beatrice (watatu kushoto) na wa kwanza kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya WIlaya ya Mpwapwa Ndugu. Paul Mamba Sweya.

Kwa upande wake mgeni rasmi Bi.Gloria Balegu, akipokea msaada huo toka kwa meneja wa Benki ya NMB tawi la Mpwapwa, amemshukuru meneja wa Benki kwa msaada huo na kuwaomba waendelee kutoa misadaa ya kijamii ili kuinufaisha na kuisaidia jamii ya watanzania.

Vile vile Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa ameupongeza uongozi wa benki ya NMB tawi la Mpwapwa kwa kuona umuhimu wa kuungana nasi katika kufanya usafi katika mazingira ya Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa na kutoa msaada wa vifaa hivyo vilivyopokelewa na Afisa Tarafa kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa.


        Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya WIlaya ya Mpwapwa Ndugu. Paul Mamba Sweya (wa kwanza kulia) akishukuru Benki ya NMB kwa kutoa vifaa vya Usafi katika Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa

Mwisho Mganga Mkuu wa Wilaya  Daktari Said Mawji amemshukuru meneja wa NMB kwa kuichagua Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa na kuipatia msaada huo wa vifaa vya usafi, hii inaonyesha kwa jinsi gani NMB imegushwa na masuala ya afya. Kwa ujumla Mazingira safi ni maisha yetu, mazingira safi ni uhai wetu, mazingira safi ni afya yetu, mazingira safi ni uchumi wetu, hivyo kila mmoja wetu ajitafakari namna anavyoweza kuwa na mchango chanya katika kuyaweka mazingira yetu katika hali ya usafi. Ikumbukwe usafi ni ustaarabu sharti uanze na mimi.

Kwa taarifa zaidi pakua nyaraka hizi.

HOTUBA SIKU YA USAFI DUNAINI SEPTEMBA 2018.pdf

HISTORIA YA USAFI DUNIANI.pdf

Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye usahili MpwapwaDC June 27, 2022
  • Tangazo la nafasi za kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa. 2022 April 20, 2022
  • Tangazo la Nafasi za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa May 2022 May 31, 2022
  • Tangazo la kuahirishwa kwa Usahili Halmashauri ya Mpwapwa June 22, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • NORISH NA WAKULIMA WILAYA YA MPWAPWA

    May 06, 2025
  • VIONGOZI KUTOKA OFISI YA MAKAMU WA RAIS ZANZIBAR WATEMBELEA MIRADI YA MFUKO WA JIMBO MPWAPWA

    May 09, 2025
  • FUM YAFANYA ZIARA MIRADI YA KIMAENDELEO

    April 29, 2025
  • MAADHIMISHO YA MEI MOSI YAFANYIKA SINGIDA

    May 01, 2025
  • Tazama zote

Video

Video ya Mpango wa Uuzaji wa Viwanja Eneo la Mazae Block "E" katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa -2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa
  • Muundo wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani
  • Ratiba ya Vikao vya Madiwani

Viunganishi Linganishi

  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Wizara ya Fedha na Mipango
  • Utumishi portal
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu Teknolojia na Sayansi
  • Sekretarieti ya Ajira

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mpwapwa - Dodoma, Tanzania

    Anwani: S.L.P 12

    Simu: 255 26 2320122/2320

    Simu ya Kiganjani: 0684705551

    Barua pepe: info@mpwapwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovutii

Copyright © 2021 Mpwapwa District Council . All rights reserved.