• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mpwapwa District Council
Mpwapwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
        • Fedha
        • Biashara
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Mali asili
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Usafi na Mazingira
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Habari Mawasiliano na Tehama
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Nyuki
    • Mamlaka
      • Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mpwapwa
      • Mamlaka ya Maji Mpwapwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashuri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa mbali mbali
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo mbali mbali
    • Simulizi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video mbali mbali
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Watoto Walalamikia Masuala Mbalimbali Yanayofanywa na Watu Wazima.

Posted on: June 16th, 2021

Watoto wa Wilaya ya Mpwapwa leo katika kuadhimisha Sherehe za Siku ya Mtoto Afrika wamelalamikia mambo mbalimbali yanayofanywa na watu wazima ambayo kwa namna moja au nyingine yanaathiri ukuaji wao kiakili, kisakolojia, kimwili na kiroho. Baadhi ya mambo yaliyolalamikiwa ni pamoja na wanawake kutoa mimba au kutupa watoto baada ya kujifungua, kutoa adhabu kali kwa watoto wanapokosea mpaka kusababisha kupoteza maisha au kupata kilema kwa baadhi ya watoto, mimba na ndoa za utotoni, na kuwanyima haki ya msingi kama kwenda shule kwa kuwapa kazi za kuuza biashara.

Akisoma risala Mwanafunzi kutoka Shule ya Sekondari Ihala kwa Mgeni rasmi Ndugu. Obert Mwalyego Afisa Tarafa ya Mpwapwa Mjini akimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Jabir Shekimweri ambaye alikuwa katika majukumu mengine ya kiserikali, imeelezwa kuwa "Katika kusherekea siku hii ya Mtoto Afrika inakumbukwa kuwa mwaka 1992 watoto zaidi ya elfu moja waliua na Makaburu huko Afrika ya Kusini katika mji wa SOWETO baada ya watoto kufanya maandamano ya kupinga kubadilishwa kwa mtaala wa masomo kuwa kwa lugha ya kigeni". Pia katika risala hiyo imeeleza kuwa katika Nchi yetu ya Tanzania watoto wanafanyiwa ukatili wa kubakwa, kupewa adhabu kali, kulawitiwa, kufanyishwa kazi  ngumu, kutopewa muda wa kucheza na kupumzika. 

Mgeni rasmi Ndugu. Obert Mwalyego (katikati) akiwa na Mkuu wa idara ya Maendeleo ya Jamii Ndugu. khamlo Njovu (kulia) na Mhe. Madanya diwani wa Kata ya Mazae (kushoto)

Hata hivyo katika sherehe hizo watoto waliamua kubeba mabango yaliokuwa na ujumbe kama Mtoto ana haki ya kuishi, kuendelezwa, kulindwa, kushirikina kutobaguliwa ili kuweza kufikisha ujumbe kwa wazazi na walezi wanao wanyima haki zao za msingi.

Aidha katika maigizo yaliyotolewa na wanafunzi kutoka Shule ya Msingi  Chazungwa Juu ya Ukali wa Watoto: Mwanafunzi anaomba fedha ya ada ya shule, baba mzazi anamtukana mtoto na kumwambia kama anataka aache shule maana haoni umuhimu wa shule, shuleni pia mwanafunzi huyo anatolewa darasani na kupewa adhabu ya viboko kwa kukosa ada wakati jukumu la kulipaada ni la mzazi. Kwa kuliona hilo ndio maana Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imefuta michango ya ada kuanzia shule ya msingi hadi kidato cha nne kwa kuwajali watoto.

Mgeni rasmi na mea kuu wakipiti kila meza kujionea kazi za sanaa zinazofanywa na watoto wa Mpwapwa

Vile vile katika igizo lilitolewa na Wanafunzi wa Shule ya Msingi Mazae Juu ya Haki za Watoto: Igizo lilionyesha kuwa kunabaadhi ya wazazi huwakataza watoto wao wasiendeshule na kuwatuma kuuza biashara ili kupata kipato cha familia wakati baba na mama wakiwa wameenda shamba kulima. Pia katika igizo hilo mwanafunzi alitambua haki zake  na kwenda polisi akiwa anauza vitumbua kuwashitaki wazazi wake ili wasiwe wanamtuma kufanyabiashara  na kumkataza kwenda shule. Hatimaye mwanafunzi alipata haki ya kuhudhurua shule na kufaulu vizuri.

Katika sherehe hizo watoto walionyesha kazi za sana za mikono kama kufuma vitambaa, kushona viatu na kucheza muziki. Kwa kutambua watoto wanapaswa kuwa wabunifu na kupata muda wa kucheza, katika siku hii watoto wamefurahi kuwa kuimba na kuonyesha vipaji vya kusoma na kucheza.

Watoto wakiwa katika igizo la Ukatili Dhini ya Watoto mbele ya meza kuu

Mwisho mgeni rasmi ameagiza vyombo vya dola na mamlaka zinazoshughulikia haki za watoto kuwasikiliza, kuwaelimisha na kuwapa msaada wanapohitaji. Pia kuwachukulia hakua watakaowafanyia ukatili watoto pamoja na wale watakaowanyima haki zao.


Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye usahili MpwapwaDC June 27, 2022
  • Tangazo la nafasi za kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa. 2022 April 20, 2022
  • Tangazo la Nafasi za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa May 2022 May 31, 2022
  • Tangazo la kuahirishwa kwa Usahili Halmashauri ya Mpwapwa June 22, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • NORISH NA WAKULIMA WILAYA YA MPWAPWA

    May 06, 2025
  • VIONGOZI KUTOKA OFISI YA MAKAMU WA RAIS ZANZIBAR WATEMBELEA MIRADI YA MFUKO WA JIMBO MPWAPWA

    May 09, 2025
  • FUM YAFANYA ZIARA MIRADI YA KIMAENDELEO

    April 29, 2025
  • MAADHIMISHO YA MEI MOSI YAFANYIKA SINGIDA

    May 01, 2025
  • Tazama zote

Video

Video ya Mpango wa Uuzaji wa Viwanja Eneo la Mazae Block "E" katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa -2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa
  • Muundo wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani
  • Ratiba ya Vikao vya Madiwani

Viunganishi Linganishi

  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Wizara ya Fedha na Mipango
  • Utumishi portal
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu Teknolojia na Sayansi
  • Sekretarieti ya Ajira

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mpwapwa - Dodoma, Tanzania

    Anwani: S.L.P 12

    Simu: 255 26 2320122/2320

    Simu ya Kiganjani: 0684705551

    Barua pepe: info@mpwapwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovutii

Copyright © 2021 Mpwapwa District Council . All rights reserved.