Hayo yamebainishwa leo Januari 30,2026 na Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe Richard Maponda wakati wa hafla ya utoaji mikopo ya10% kwa robo ya pili 2025/2026 katika Ukumbi wa Halmashauri.
Mhe Maponda amewataka wanavikundi hao watakaopatiwa mkopo huo kuurejesha kwa wakati ili uweze kutembea kwa wengine,na kusisitiza kuwa pindipo wanavikundi watakuwa na sifa nzuri ya kurejesha mkopo na kukopa wataweza pata nafasi nyengine kwa kipindi kijacho.
Hata hivyo amesema pindipo hutokuwa na sifa ya kukopa na kurejesha kwa wakati basi utakopa mara tu lakini watahakikisha umeresha na hutokopeshwa tena.
Halikadhalika, amewataka wanavikundi hao kuwaheshimu viongozi wao wanaowasimamia ambao ni Maafisa Maendeleo na kupokea maelekezo yake anayoyatoa,yasimamiwe na yatekelezwe vizuri.
"Nitumie nafasi hii niwaombe sana,nyinyi ambae leo tupo pamoja nanyi niwambe mrejeshe mikopo yenu ili mikopo itembee"
"Namkiwa na sifa nzuri ya kurejesha mikopo na kukopa tutakupa nafasi ya kukopa hadi kipindi kinachofuata".Amesema Mhe Maponda
Jumla ya Vikundi 32 vimepatiwa mkopo ikiwa 18 vya wanawake na 14 vya vijana,na Jumla ya Shililing 228,500,000.00 zimetolewa kwa wanavikundi hao.










Mpwapwa - Dodoma, Tanzania
Anwani: S.L.P 12
Simu: 255 26 2320122/2320
Simu ya Kiganjani: 0684705551
Barua pepe: info@mpwapwadc.go.tz
Copyright © 2021 Mpwapwa District Council . All rights reserved.