Mhe Dkt Sophia M Kizigo Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Leo Disemba 11,2025 akiambatana na kamati kuu ya ulinzi na Usalama Wilaya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji Bi Mwanahamisi H Ally na ofisi yake amefanya ziara ya kukagua miradi ya kimaendeleo inayoendelea kujengwa wilayani mwake.
Wakati wa ziara yake hiyo amekagua mradi wa Ujenzi wa Ofisi Mpya ya Halmashauri uliofika hatua ya pili ya ujenzi wake,amekagua maabara na vyoo vya shule ya Sekondari ya Amali Mmbuyuni,amekagua nyumba ya Mkurugenzi na za wakuu wa Idara Mazae pamoja na majengo ya vyoo vya Shule ya Msingi Igovu.
Mhe Kizigo amewataka wasimamizi wa miradi hiyo waengeze kasi za kazi zao ili waendane na muda waliopewa.







Mpwapwa - Dodoma, Tanzania
Anwani: S.L.P 12
Simu: 255 26 2320122/2320
Simu ya Kiganjani: 0684705551
Barua pepe: info@mpwapwadc.go.tz
Copyright © 2021 Mpwapwa District Council . All rights reserved.