• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mpwapwa District Council
Mpwapwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
        • Fedha
        • Biashara
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Mali asili
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Usafi na Mazingira
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Habari Mawasiliano na Tehama
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Nyuki
    • Mamlaka
      • Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mpwapwa
      • Mamlaka ya Maji Mpwapwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashuri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa mbali mbali
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo mbali mbali
    • Simulizi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video mbali mbali
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Mkuu wa Wilaya Aridhishwa na Ujenzi wa Kituo cha Afya

Posted on: January 7th, 2019

(Na: Shaibu J. Masasi, Afisa TEHAMA - Mpwapwa)

Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Jabari Shekimweri ameridhishwa na kasi ya ujenzi wa kituo cha Afya Kibakwe katika hatua ya umaliziaji. Katika ziara ya leo amekagua madirisha, milango, masinki ya kunawia maji, umaliziaji wa plasta katika baadhi ya majengo, umaliziaji wa vigae vya sakafuni (tiles) na umeme. Akipongeza hatua iliyofikiwa kwa sasa Mhe. Shekimweri amesema "katika ziara yangu ya tarehe 31 Desemba, 2018 nilibaini mapungufu kadha na nilitoa maagizo ambayo yametekelezwa, hivyo nimeridhishwa na hatua hii".

Pia Mkuu wa Wilaya ametoa agizo kuwa jengo la kuhifadhia maiti halina milango, hivyo ifungwe mara moja na Alhamisi tarehe 10 Januari, 2019 iwe mwisho.

Jengo la Wodi ya Wazazi katika Kituo cha Afya Kibakwe Ambalo lipo katika hatua za mwisho kukamilishwa

Katika hatua nyingine Mhe. Shekimweri ameridhishwa na hatua ya ukamilishaji wa miundombinu ya umeme katika nyumba ya mganga ambapo katika ziara yake iliyopita alitoa siku tano kwa Fundi Umeme Ndug. Michael Lubaja kukamilisha kazi hii na fundi alikamilisha kama alivyoagizwa. Kukamilisha kazi hii kwa wakati imesababisha Mkuu wa Wilaya kufurahi na kuomba wajumbe waliohudhuria kumpigia makofi ya sifa fundi umeme huyo kwa kukamilisha kazi iliyobaki ndani ya siku tano.

Jengo la Nyumba ya Mganga katika Kituo cha Afya Kibakwe Ambalo lipo katika hatua za mwisho kukamilishwa

Kwa upande mwingine, katika mradi wa ujenzi wa madarasa katika Shule ya Sekondari Kibakwe ambapo kwa sasa yapo katika hatua ya madirisha. Katika hatua hii Mkuu wa Wilaya amesifu kasi inayoendelea na kusitisha wazo lake alilotoa katika ziara ya awali kuwa angeliwaleta Askari wa JKT kuja kusaidia kazi ya ujenzi wa madarasa kwa kuwa kasi ya ujenzi ni ya kusuasua. Hata hivyo Fundi mkuu wa ujenzi wa madarasa na kamati yake ya ujenzi wamejipanga vizuri katika kuhakikisha wanaenda kwa kasi kwa kufuata ubora na viwango vilivyoaanishwa.

Mkuu wa Wilaya amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa Ndug. Paul Mamba Sweya kuhakikisha madirisha, milango, mbao na bati zinaandaliwa mapema katika ujenzi wa madarasa katika Shule ya Sekondari Kibakwe ili kazi hii isisimame kwa kukosa vifaa.

Aidha ziara ya Mkuu wa Wilaya ilielekea Kata ya Gulwe ambako kunajengwa shule ya Sekondari Gulwe kwa nguvu za wananchi kwa kuhamasishwa na viongozi wa kata hiyo akiwemo diwani  kwa kufyatua tofali, kusomba mchanga, maji , mawe, na kujitolea maeneo ya kujenga shule. Pia wamewahamasisha wananchi wachangie fedha ambapo mpaka sasa Shilingi Milioni Kumi na elfu themanini na mbili tu (Tsh.10,082,000/=).Ujenzi kwa sasa umefikia katika hatua ya madirisha na unaendelea ambapo madarasa matatu yamefikia hatua ya lenta ambapo jengo moja lenye madarasa limefikia hatua ya madirisha.

Ujenzi wa Shule ya Sekondari Gulwe

Mkuu wa Wilaya ameagiza kuwa ili kutatua migogoro ya ardhi wananchi waliotoa aridhi kwa ridhaa yao kuwe na makubaliano ya maandishi, eneo hili la shule lipimwe na liwe na hati. Mkuu wa Wilaya ameuliza kama wasimamizi wa ujenzi wa shule wamejiridhika kama majengo hayapo katika hifadhi ya barabara, Mwenyekiti wa kijiji amejibu kuwa wataalam wamejiridhisha kuwa majengo hayapo katika hifadhi ya barabara.

Mhe. Shekimweri amewapongeza sana viongozi wa kata pamoja na wananchi kwa ujumla kwa kujitoa kwa ajili ya kuanziasha ujenzi wa shule ya sekondari ya Gulwe baada ya kuona watoto wao wanasoma kata za mbali ikiwepo Mazae, Vinghawe na Mpwapwa Mjini. Tunaomba viongozi muendelee na hamasa kama hii, amesisitiza Mkuu wa Wilaya.

Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye usahili MpwapwaDC June 27, 2022
  • Tangazo la nafasi za kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa. 2022 April 20, 2022
  • Tangazo la Nafasi za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa May 2022 May 31, 2022
  • Tangazo la kuahirishwa kwa Usahili Halmashauri ya Mpwapwa June 22, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • NORISH NA WAKULIMA WILAYA YA MPWAPWA

    May 06, 2025
  • VIONGOZI KUTOKA OFISI YA MAKAMU WA RAIS ZANZIBAR WATEMBELEA MIRADI YA MFUKO WA JIMBO MPWAPWA

    May 09, 2025
  • FUM YAFANYA ZIARA MIRADI YA KIMAENDELEO

    April 29, 2025
  • MAADHIMISHO YA MEI MOSI YAFANYIKA SINGIDA

    May 01, 2025
  • Tazama zote

Video

Video ya Mpango wa Uuzaji wa Viwanja Eneo la Mazae Block "E" katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa -2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa
  • Muundo wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani
  • Ratiba ya Vikao vya Madiwani

Viunganishi Linganishi

  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Wizara ya Fedha na Mipango
  • Utumishi portal
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu Teknolojia na Sayansi
  • Sekretarieti ya Ajira

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mpwapwa - Dodoma, Tanzania

    Anwani: S.L.P 12

    Simu: 255 26 2320122/2320

    Simu ya Kiganjani: 0684705551

    Barua pepe: info@mpwapwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovutii

Copyright © 2021 Mpwapwa District Council . All rights reserved.