• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mpwapwa District Council
Mpwapwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
        • Fedha
        • Biashara
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Mali asili
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Usafi na Mazingira
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Habari Mawasiliano na Tehama
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Nyuki
    • Mamlaka
      • Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mpwapwa
      • Mamlaka ya Maji Mpwapwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashuri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa mbali mbali
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo mbali mbali
    • Simulizi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video mbali mbali
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa Ajipanga Kumalizia Ujenzi wa Ukumbi Uliokwama Tangu Mwaka 2014

Posted on: November 13th, 2020

Na: Shaibu J. Masasi, Afisa TEHAMA - Mpwapwa Dc

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa Ndugu Paul Mamba Sweya leo amemualika Kaimu Mkurugenzi wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Mhandisi Alinanuswe Mwakiluma akiwa na timu yake ya Wasanifu wa Majengo na wahandisi kuja kukagua Jengo la Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa ambalo ujenzi wake ulikoma tangu mwaka 2014. 

Kihistoria Jengo la Ukumbi wa Halmashauri ya Mpwapwa lilianza kujengwa tarehe 28 Machi 2013 kwa mujibu wa Mkataba namba LGA/023/CDG/W/QT/2012/13/01 na Kampuni ya Magoma & Lyatimbo Construction LTD ya Dar ES Salaam kwa thamani ya Tsh. 356,500,000/= hadi jengo kukamilika. Jengo hilo kama lingekamilika lilitakiwa kuwa na Ukumbi wa mikutano, Ofisi za Mwenyekiti wa Halmashauri, Mkamamu mwenyekiti wa Halmashauri na Mwandishi wa Mikutano ya Halmashauri.

Jengo la Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa lilipoishia tangu Mwaka 2014 Hadi sasa.


Dhumuni la kuwaita wataalam toka TBA ni kuja kupima na kutathmini kama jengo hilo bado lina uwezo wa kuendelezwa kujengwa ili Halmashauri ya Willaya ya Mpwapwa iendelee kujenga au kama lina kasoro, hivyo libomolewe na ujenzi uanze upya.

Akizungunza katika Utambulisho wa wataalam hao Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa Ndugu Sweya, amesema "Tumewaita hawa wataalam ili waje kupima na kutushauri kwa maandishi kama tunaweza kuendelea na ujenzi au jengo halina nguvu ya kuhimili muendelezo wa ujenzi kwa kuwa jengo hilo lilijengwa muda mrefu na halikumaliziwa tangu mwaka 2014 mpaka sasa, hivyo Halmashauri ya Wilaya imeona ipo haja ya kumalizia ili tuwe na ukumbi wa kisasa hata Viongozi toka Makao Makuu ya Nchi Dodoma siku moja waweze kufanyia vikao vyao Mpwapwa ". Ndugu Sweya ameongeza kuwa "Hapa Mpwapwa hakuna Ukumbi wa Kisasa hivyo kumalizika kwa ukumbi huu utawezesha upatikanaji wa mapato kwa kukodisha kwa ajili ya sherehe na mikutano ya jamii".

Timu ya Wataalam toka TBA na Halmashauri wakikagua Jengo la Ukumbi (Wakwanza Kushoto - Mhandishi Mwakiluma toka TBA  na Wapili Kushoto - Ndugu Paul Sweya, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa)


Nae, Kaimu Mkurugenzi wa TBA Mhandishi Mwakiluma amempongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mpwapwa kwa kuchukua jitihada za kutaka kumalizia jengo hili, na amekiri kuwa jengo ni la muda mrefu na wamekuja na kifaa maalau kinachojulikana kwa jina la kitaalam kama Rebound Hummer kwa ajili ya kupima ubora wa jengo katika maeneo muhimu kama kwenye nguzo na bim ili kubaini kama jengo bado lina uwezo wa kuhimili mwendelezo wa ujenzi. 

Mhandisi Mwakiluma amesema "Kazi ya leo ni kupima tu na kuchukua data toka katika kifaa maalam ndio maana mnaona hapa tunapiga kama risasi  katika maeneo ya nguzo na bim baada ya zoezi hili tutawaletea taarifa ya maandishi ambayo ndio itaamua kama jengo lote libomolewe au ujenzi uendelee ".

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa Ndugu Sweya (kulia) akiwaonyesha wataalam maeneo ya Jengo la Ukumbi huo


Baada ya zoezi la kukagua jengo na kuchukua vipimo kukamilika Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mpwapwa ameishukuru Timu nzima ya TBA kwa kuitikia wito na kuja kufanya kazi hii nzuri kwa ushirikiano mkubwa.

****Mwisho****

Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye usahili MpwapwaDC June 27, 2022
  • Tangazo la nafasi za kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa. 2022 April 20, 2022
  • Tangazo la Nafasi za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa May 2022 May 31, 2022
  • Tangazo la kuahirishwa kwa Usahili Halmashauri ya Mpwapwa June 22, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • NORISH NA WAKULIMA WILAYA YA MPWAPWA

    May 06, 2025
  • VIONGOZI KUTOKA OFISI YA MAKAMU WA RAIS ZANZIBAR WATEMBELEA MIRADI YA MFUKO WA JIMBO MPWAPWA

    May 09, 2025
  • FUM YAFANYA ZIARA MIRADI YA KIMAENDELEO

    April 29, 2025
  • MAADHIMISHO YA MEI MOSI YAFANYIKA SINGIDA

    May 01, 2025
  • Tazama zote

Video

Video ya Mpango wa Uuzaji wa Viwanja Eneo la Mazae Block "E" katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa -2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa
  • Muundo wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani
  • Ratiba ya Vikao vya Madiwani

Viunganishi Linganishi

  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Wizara ya Fedha na Mipango
  • Utumishi portal
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu Teknolojia na Sayansi
  • Sekretarieti ya Ajira

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mpwapwa - Dodoma, Tanzania

    Anwani: S.L.P 12

    Simu: 255 26 2320122/2320

    Simu ya Kiganjani: 0684705551

    Barua pepe: info@mpwapwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovutii

Copyright © 2021 Mpwapwa District Council . All rights reserved.